Habari za Punde

Rais Mpya wa TFF Afuatilia Mchezo wa Kirafiki wa Simba na Mlandege Uwanja wa Amaan Zanzibar.

Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
Rais mpya wa Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF) Walace Karia alikuwa mmoja kati ya watu waliohudhuria mchezo wa kirafiki kati ya Simba dhidi ya Mlandege ambao ulipigwa jana saa 2 za usiku katika uwanja wa Amaan timu hizo zikitoka sare ya 0-0.2
Jumamosi iliyopita ya Agost 12, 2017 Karia alishinda Urais wa TFF baada ya kupata kura 95 kati ya 128 za wajumbe waliopiga kura kwenye uchaguzi huo uliofanyika Mjini Dodoma.
Karia amewashinda Iman Madega, Shija Richard, Ally Mayay, Emanuel Kimbe na Fredrick Mwakalebela ambao walikuwa wakiwania nafasi ya urais wa TFF.
Kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais wa TFF, Karia alikuwa makamu wa Rais chini ya Jamal Malinzi ambapo baadae aliendelea kuiongoza TFF baada ya Malinzi kuwa mahabusu akikabiliwa na mashitaka ya matumizi mabaya ya ofisi.

Karia ataongoza shirikisho la soka Tanzania kwa kipindi cha miaka minne kwa mujibu wa katiba ya TFF.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.