Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Shein Amtumia Salamu za Pongezi Rais wa Jamuhuri ya Watu China Kuadhimisha Miaka 68.

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                                                              26.09.2017
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping kwa kutimiza miaka 68 tokea kuasisiwa kwa Taifa hilo.

Katika salamu hizo, Dk. Shein alimpongeza Rais Xi Jinping kwa kutimiza miaka 68 ya Taifa hilo tokea kutangazwa rasmin na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Kikomunisti cha Jamhuri ya Watu wa China Hayati Mao Zedong mnamo Oktoba 1, mwaka 1949.

Salamu hizo zilieleza kuwa wananchi wa Zanzibar wataendeleza umoja na mshikamano walionao kati yao na ndugu zao wa Jamhuri ya Watu wa China kwa lengo la kuendeleza uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya pande mbili hizo.

Aidha, katika salamu hizo, Dk. Shein alimtakia sherehe njema kiongozi huyo wa Jamhuri ya Watu wa China pamoja na wananchi wake wote sambamba na kuendeleza amani na utulivu iliyopo nchini humo pamoja na kuimarisha zaidi mafanikio yaliopatikana katika sekta za uchumi na maendeleo.

Dk. Shein katika salamu hizo, alieleza kuwa katika miaka 68 tangu kuasisiwa kwa Taifa hilo, Jamhuri ya Watu wa China imeweza kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa kudumu kati yake na Zanzibar.

Sambamba na hayo, Dk. Shein alimtakia kiongozi huyo pamoja na familia yake na wananchi wote wa Jamhuri ya Watu wa China afya njema, na mafanikio zaidi katika kuuimarisha uchumi wao ambao umekuwa ukiimarika siku hadi siku sambamba na maendeleo yaliopo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.