Habari za Punde

Wakuu wa Idara za Serikali watakuwa kuwa wakweli na wawazi

Na Masanja Mabula - Pemba


SERIKALI ya  Mkoa wa Kaskazini Pemba  imeanza kutekeleza kwa vitendo maagizo ya   Rais wa Zanzibar kwa kugawa  majukumu ya utekelezaji wa maagizo  hayo kwa  maofisa  Wadhamini wa Wizara na taasisi za Serikali Kisiwani Pemba.

Akizungumza katika kikao cha kutathmini ziara ya   Rais katika Mkoa huo , Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba  Omar Khamis Othman amewataka wakuu wa Idara za Serikali kuwa wakweli na wawazi ili kuendana na kasi ya utendaji wa Rais kwa kuhakikisha maagizo hayo wanayafanyia kazi .

Amesema kila Wizara inapaswa kushiriki katika kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo yaliyotolewa na Rais wakati wa ziara yake mwezi uliopita katika Mkoa huo.

“Ni vyema kila mmoja anatakiwa kuwajibika kusimamia utekelezaji wa maagizo ya Rais Shein aliyoyatoa wakati wa ziara yake katika Mkoa wetu , hii itasaidia kwenda kasi na Rais wetu ”alieleza.

Wakichangia katika kikao baadhi ya maofisa wadhamini wamesema tayari wameanza kuyafanyia kazi maagizo  ya  Rais kwa kufanya ziara na mikutano ya watendaji wa taasisi zao.

Mapema Katibu Tawala Mkoa wa Kaskazini Pemba Ahmed Khalid Abdalla amewapongeza maofisa wadhamini kutokana na mchango wao uliofanikisha ziara ya  Rais katika mkoa huo .


Naye Mkuu wa Wilaya ya Wete Rashid Hadid Rashid amewasisitiza wakuu hao wa taasisi kuhakikisha wanawajibika katika kutekeleza maagizo ya Rais kwa uwazi ili wananchi wazidishe imani na serikali yao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.