NA HAJI NASSOR, PEMBA
JESHI la Polisi mkoa wa kusini Pemba, linamtafuta kijana
Mohamed Nassor (25) mkaazi wa Changaweni wilaya ya Mkoani, akituhumiwa
kumtorosha msichana (16), aliechini ya uangalizi wa wazazi wake.
Kamanda
wa Polisi Mkoani humo, Shehan Mohamed Shehan, alisema kijana huyo, alitoroka
baada ya kushitukia kuwa anafautwa na Polisi, baada ya kufanya kosa hilo.
Alisema
kijana huyo alikwenda kijiji cha Makombeni Oktoba 23, na alipofika, alimtorosha
msichana huyo na kumpeleka Changaweni kwa lengo la kumingilia.
Alisema
baada ya mtoto huyo kuhojiwa, ndipo taarifa zilipowafikia na kuanza kumtafuta,
ingawa taarifa za awali zilionyesha amekimbia.
“Jeshi
ka Polisi linamtafuta kila kona, na limeshaweka mitego, ili kuhakikisha
anapatikana na kufika mbele ya mkono wa sheria kujieleza”,alisema.
Hata
hivyo amewataka wazazi na walezi, kuwa karibu na watoto wao, na kila baada ya
muda kujua walipo, ili kuweza kutatua changamoto kama hizo zinapowatokea.
Wakati
huo huo Jeshi hilo la Polisi Mkoani humo, linaendelea kumuhoji kijana Juma
Abdalla Salum (29), mkaazi wa mjini Chakechake, kwa tuhuma za kumuingilia
Ng’ombe jike.
Alisema
kijana huyo alietenda kosa hilo Oktoba 23, majira ya saa 12:30 jioni eneo la
Ngoma hazingwa nje kidogo ya mjini wa Chakechake,ambapo alionekana na watu na kisha kufikishwa Polisi.
Kamanda
Shehan alisema, baada ya kufikishwa Jeshi la Polisi linaendele kumuhoji na
ikiwa ataonekana anahusika na tukio hilo, jalada lake litafikishwa kwa DPP kwa
ajili ya uchunguzi na kisha kupanda mahakamani.
“Tukimaliza
taratibu za kumuhoji, linalofuata ni kufikishwa mahakamani kwa ajili ya kujibu
tuhuma zinazomkabili za kumuharibu mnyama”,alifafanua.
Hili
ni tukio la pili kwa mwaka huu wa 2017, la kumuingilia mnyama, ambapo tukio la
kwanza lililtokea miezi minne iliopita, shehia ya Vitongoji wilaya ya
Chakechake.
No comments:
Post a Comment