ALIEKUWA dereva wa gari ya wizara ya
Afya kisiwani Pemba Suleiman Mohamed Suleiman (74), akizungumza na mwandishi wa
habari wa makala wa Shirika la Magazeti ya Serikali Pemba, Haji Nassor Mohamed
(kulia), juu ya hali ya afya yake baada ya kustaafu, (Picha na Habiba Zarali, Pemba)
-Msongo
wa mawazo, bawasili, kuchanika mifupa ni rundo la mgonjwa yanayowapata madereva
-Wa
serikali watajwa kunyemelewa zaidi hasa wakinyimwa likizo
NA HAJI NASSOR, PEMBA
“KAMA dereva hawezi kufanya
mazoezi, basi walau inapolala gari na yeye, pawe na masafa wa kuifuata walau
dakika 30” ndio kauli ya mtaalamu wa magonjwa ya mifupa dk Rahila wa hospitali
ya Chakechake Pemba.
Anasema,
kinga kubwa ya magonjwa hayo, moja wapo kwa maderava hasa wa serikali, ni
kufanuya mazoezi, lakini kama wanashindwa wanatakiwa kila siku, waifuate gari
kutoka anapolala kwa dakika 15 hadi 30.
Sio
sahihi dereva anapoishi, na nje ndio pana gari tena ya ofisi, dereva wa aina hii,
ndie wa kwanza kukumbwa na magonjwa kati ya yale nane yanayoweza kuwapata.
Tena
ogopa zaidi dereva hasa wa gari ya serikali, kisha anatumia vinywaji kama
pombe, na kahawa kwa wingi au sigara, na kisha gari ya ofisini anaifanya kama
ibada haishuki.
“Wapo
madereva kwanza niwatumiaji wa pombe, kahawa kwa wingi, au wanavuta sigara, na
gari ya ofisini anauhuru nayo wakati wowote, na kuwaona wenzake mabwege kwa
kuny’ang’anywa gari baada ya saa za kazi, ajue kuwa magonjwa yanamnyelea’’,anasema
dk Rahila.
Magonjwa
matatu (3) ndio pekee ambayo yanaweza kumpata dereva hasa wa gari za serikali
kwa kule, kukaa kwao sana kwenye usukani, moja ni msongo wa mawazo (stress).
Mtaalamu
huyu, anasema msongo huu wa mawazo kwa madereva hasa wa serikali, husababishwa
na mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na uchakavu wa gari, kukoseshwa likizo na hata
kutopewa fedha za baada ya saa kazi ‘overtime’
“Dereva
anamiaka zaidi ya mitano au zaidi yeye yuko kwenye usukani bila ya kupewa
likizo, huku gari mbovu, hana fedha za ziada za muda wa saa baada ya kazi,
kisha anamuendesha kiongozi hapa lazima ‘stress’imuandame”,anasema.
Lakini
maradhi mengine ambayo yanaweza kuwapata madereva wote wakiwemo wa serikali, ni
mifupa yake kuchanika bila ya kupata ajali, ambapo hili hujitokeza baada ya
zaidi ya miaka mitano, ingawa inategemeana na afya ya dereva mwenyewe.
Imezoeleka
kuwa, mtu hawezi kuvunjika mfupa mpaka apate ajali, ingawa kwa madereva
wanaoendesha gari kwa muda mrefu bila ya kupumzika, ndio ambao hukumbwa na hali
hii.
“Unajua
madereva wa serikali kuanzia siku ya kwanza wanaoajiriwa hadi siku anastaafu,
ofisi yake ni ndani ya gari, ambapo humu hapati kulala (wima), yaani mifupa na
viungo havikunjuki, hivyo uwezekano wa kuvunjika na kuchanika upo”,anafafanua.
Njia
ya uvujikaji wa mifupa ya mikono ni kule kuizungurusha mifupa ya mikono yake wakati
anapoipindisha sukani ya gari au kakanyaga klachi, au hata kitufe cha breki.
“Wapo
wamekaa kama magolkipa wa muda mrefu, maana kama waliopinda kwenye sehemu ya
kuanzia nyongani hadi mikononi, kwa kule kuilalia sukani muda mrefu bila ya
mapunziko”,anaeleza.
Dereva
wa aliekuwa wizara ya Afya Pemba, Suleiman Mohamed Suleiman (74), mkaazi wa
mjini Chakechake, anasema baada ya kustaafu, anajihisi maumivu makali, kwenye
maoteo ya miguu miwili.
Anajihisi
maumivu ambayo kwa sasa hayamruhusu kusimama wima, wakati anapotembea, akiamini
kuwa kitako alichokaa tokea mwaka 1977, akiwa dereva wa wizara hiyo, hadi
alipostaafu mwaka 2012 ndio sababu.
“Mimi
nimeendesha gari kwa miaka 35 mfululizo bila ya likizo, hivyo ilifika wakati
naendesha gari nikiwa na machofu, maana nilipoomba likizo, niliambiwa
wafanyakazi ni haba sektaya udereva, hivyo nivumilie”,anasema.
Mzee
Suleiman, ambae kwa sasa ni mkulima na akiwa na biashara ya vinywaji karibu na
maegesho ya gari ya Gombani ndani ya mji wa Chakechake, anasema wala hakumbuki
siku aliopewa fedha za baada ya saa kazi “over time” ingawa anasema hakuna siku
aliorudi kwake mapema.
Kitaalamu
kila dereva anapokuwa barabarani huwa anachunga gari nne moja ni ile ilio
kuliani kwake, kushoto, mbele na nyuma, hukuwa pia akiwa na tahadhari kwa
aliowabeba ili gari isiingie shimoni.
Ambapo
hayo yote, kama nae hakuangaliziwa haki zake uwezekano wa kutokezea ajali au
kuchoka mapema kwenye kazi yake hiyo huweza kujitokeza wakati wowote.
“Siku
moja siisahu mwaka 1999 ilikuwa jioni, nilipata ajali nikiwa nimebeba madaktari,
baada ya mpira wa mbele kupasuka “tairi”, tena kama jana nilishatoa taarifa
ofisini, lakini unajua tena, mpaka litokee”,alinikumbusha mzee Suleiman.
Dk
Rahila anasema uongonjwa mwengine ambao unaweza kumpata dereva hasa asiepata
mapunziko ni bawasili, yaani kutoka mithili ya nyama kwenye sehemu ya haja
kubwa, kunakosababishwa na mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kukaa kitako muda
mrefu kwenye joto.
“Huu
ugonjwa kila mmoja humpata, kwa sababu zake mbali mbali, lakini kwa madereva
kule kukaa sana kwenye usukani na chini yao pana mashine inayozalisha joto
wasilolihitaji ni sababu”, anabainisha.
Mtaalamu
wa mashine za gari kutoka Wizara ya Miundombinu kisiwani Pemba, Mhandisi Khatib
Mkubwa Khatib, anasema mashine zote za gari hutakiwa kuwa na joto la wastani wa
78 hadi 85 sentigredi.
Anasema
gari isiofanyiwa matengenezo ya kila baada ya muda “service” joto lake aidha
houngezeka au kupanda juu zaidi, ambapo kwa hali yoyote hiyo, inaweza
kumuathiri dereva kwenye viungo vyake.
“Joto
la kawaida analotakia kuwa nalo mwanadamu ni kati ya sentigrade 32 hadi 40,
lakini kwa dereva alie na gari mbovu anakumbana na joto mara mbili, hivyo
athari mwilini mwake humyemelea”,anafafanua.
Anasema
kitaalamu gari hutakiwa kufanyiwa uchunguuzi wa mashine kila baada ya mwezi,
ingawa hutegemeana na safari zake, yote hayo ni kumkinga dereva asipate madhara
yatokanayo na kazi yake.
Khamis
Sultan Hemed (67) alieajiriwa udereva mwaka 1971 na kuendesha gari kwamiaka 29,
anasema hadi anastaafu yeye bado kiafya anajihisi mzima, ingawa changamoto
aliokumba nayo ni machofu ya kazi yake, kwakunyimwa likizo.
“Mimi
namkumbuka nimeanza kushika usukani kwa miaka 30 mfululizo, na nilipewa likizo
mwaka 2000 kwa ajili ya kustaafu, na hilo niliombwa kabla halijamalizika nirudi
kazini, na nilirudi”,anasema.
“Mwendo
wangu ni wa kusua sua kwa sasa, nahisi baadhi ya viungo havikunjuki hata nikivilamisha,
lakini tokea nilipostaafu Kamisheni ya Utalii nimepewa gari ndogo aina ya
“carry” na tajiri nadowea mwenye boksi au mzigo niusafirishe eneo
jengine”,anasema.
Kumbe
Khamis Sultan baada ya kustaafu mwaka huo wa 2000, alikaa mwaka mmoja tu nje,
ndipo mwaka 2001 alipopewa kinua mgongo chake kisichozidi shilingi 5,000,000
(milioni tano), ambapo hakuweza kujiendeleza kimaisha.
“Nimemaliza
kutumwa na serikali kwa miaka 30, na sasa natumwa na mtu binafsi mpaka niwe
sijiwezi tena, kanipa kikeri (gari ndogo inayobeba nusu tani ya mzigo), hichi
nazunguruka nacho mjini kutafuta kula”, anasema kwa unyonge.
Kimsingi
wataalamu wa afya wanakubaliana kuwa, kila kazi inahitaji mapunziko, ambayo
yataambatana na kuangaliwa kwa afya ya mfanyakazi husika, awe dereva au
mwengine.
Lakini,
kwa dereva wa alieanzia Idara ya Majenzi mwaka 1971 na kuishia Kamisheni ya
Utalii mwaka 2000 mzee Khamis Sultan anasema, hakumbuki kwenda likizo hata mara
moja, ukiachia lile la kusataafu ambalo
nalo lilikatwa.
Dereva
mwengine wa Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Ali Massoud Ali (30) alieajiriwa
mwaka 2011, anasema hadi sasa afya iko vizuri na wala hajahisi maumivu yoyote
yanayosababishwa na kazi yake.
“Mimi
niko sawa sana kiafya, ingawa sijaambiwa wapo kama leo niende hospitali
kuchunguuzwa afya yangu, maana nakumbuka wakati nataka kuajiiriwa tu, ndio
tulitakiwa kufanya hivyo”,anasema.
Tayari
ameshapata mapunziko ya likizo kwa mara nne (4), tokea alipoajiriwa, jambo
ambalo linampa kuchuma akili mpya ya kazi yake, na hadi sasa hakuna kiashiria
chochote cha magonjwa mwilini mwake.
Mohamed
Massoud Amran (30) dereva wa Shirika la Utangaazaji Zanzibar ZBC ofisiya Pemba,
alieajiriwa mwaka 2000, anasema amekwenda likizo mara tatu pekee, ingawa
hakumbuki kuomba likizo na kukataliwa.
Kwa
sasa dereva huyo, anaetimiza miaka 17 kwenye usukani, anasema tayari ameshaanza
kupata mabadiliko ya mwili, ikiwa ni pamoja na maumivu makali ya kifua.
“Ingawa
kifua sio kila siku, lakini hukaa na kinapokuja huwa na maumivu, naamini
yanatokana na vumbi na kuvuta harufu ya mafuta machafu wakati nipoingia
mvunguni kutengeneza gari”,anasema.
Lakini
dereva huyo wa ZBC kisiwani Pemba, anasema ameshaanza kuona tofauti ya uoni
wake, akiamini kuwa macho nayo yameshagonjwa kwa kuvaa miwani asioitarajia,
yaani kioo cha gari.
Magonjwa
mengine anayoyaona yanamnyelea ni pamoja na maumivu ya nyonga, miguu kuwaka
moto bila ya sababu, mikono kuhisi maumivu kwenye mifupa mitihili ya mtu
alievunjika.
Kanuni ya Utumushi wa umma
ya mwaka 2014 kwenye kifungu chake cha 5 (1) na kwa kuzingatia sheria ya
utumishi wa umma ya mwaka huo, kinaeleza wazi kuwa mtu yeyote atakaeingia
katika utumishi wa umma, atalazimika kujaza fomu inayoitwa ‘ardhilihali’
Ambapo atafanyiwa uchnguuzi
wa afya yake na kuthibitishwa iwapo afya yake, inaruhusu kufanya kazi husika,
tena awe lazima ni daktari wa serikali, katika hospitali iliokubalika.
Ingawa
moja ya mapungufu yaliomo kwenye kanuni hii na sheria yake, ni kutokuwepo
kifungu kinamcholazimisha muajiri, kumfanyia uchunguuzi wa kiafya muajiriwa
wake, kila baada ya muda, kama inavyokuwa wakati wa kutaka kumuajiri.
Mwenyekiti
wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar Jaji Mshibe Ali Bakari, anasema
mapungufu yaliomo kwenye sheria hiyo iliodumu kwa miaka 13 sasa, ndio
yaliowasukuma kutaka kuifanyia marekebisho.
“Muajiri kwa mujibu wa
sheria hii na kanunui yake, anawajibu wa kumchunguuza mtu anaetaka kumuajiri
kwenye utumishi wa umma kwa kumfanyia uchunguzi, hili ni kunyume na sasa
tunataka kuingiza kifungu cha kufanyia uchunguuzi hata akiwa kazini kila baada
ya muda”,anasema.
Ingawa kununi na sheria
hiyo, imetoa haki iwapo muajiriwa atajifanyia mwenyewe uchunguuzi na kujibaini
ana magonjwa yaliosababishwa na kazi yake, hapo muajiri (serikali) inaweza
kumtibu hadi nje ya nchi.
Nayo sheria afya na usalama
kazini no 8 ya mwaka 2005 kwenye kifungu chake cha 58, kimeweka wazi kuwa ‘kila
baada ya muda wafanyakazi, watachunguuzwa afya zao na daktari wenye sifa ambao
wataidhinishwa na Mkurugenzi’
Aidha kifungu hicho
kilifafanua kuwa, gharama za uchunguuzi huo zitalipwa na Muajiri (serikali),
ingawa wastaafu hao waliozungumza na mwandishi wa makala haya, hawakumbuki
kufanyiwa uchunguuzi huo, hadi kustaafu kwao.
Asha
Muhidini muajiriwa wa wizara ya Afya Pemba, amesema yeye mwakani anastaaafu,
ingawa hakumbuki hata siku moja kuitwa na muajiri wake, kwa ajili ya kufanyiwa
uchunguuzi.
“Ukali
na umakini wanaokuwa nao waajiri wakati wanapotaka kuajiri kwa kuwafanyia
uchunguuzi wa afya zao, basi hata baada ya kuwaajiri watekeleze sheria ya
kuwafanyia uchunguuzi”,alifafanua Asha.
Nae
Mwajuma Hassan Kombo mwalimu katika skuli moja ya sekondari Wete, ambae
hakupenda jina la skuli ichapishwe, alisema zaidi wao wanaoishi na vumbi la
chaki, ndio walipaswa kuangaliwa haraka.
“Mimi
niliomba kustaafu mapema, maana macho yalishaanza kupoteza nuru, kutokana na
kuzidiwa na vumbi la chaki, ingawa sikumbuki kuambiwa nikachunguuzwe, na hata
nilipoamua kujitibu gharama nilipoomba sikupewa”, alifafanua .
Afisa
Mdhamini wizara Ardhi, Makaazi, Maji na
Nishati Pemba, Juma Bakari Alawi, anasema anaelewa uwepo wa jukumu la
kuwafanyia uchunguuzi wa kiafya wafanyakazi wao, ingawa tatizo ni ukosefu wa
fedha za kugharamia.
“Kwenye
bajeti ijayo ya mwaka 2018/2019, tunatarajia sasa tutenge bajeti maalumu kwa
ajili hiyo, maana kweli wapo wafanyakazi wanatarajia kustaafu karibuni, lakini
hawajawahi kufanyiwa”,alifafanua.
Afisa
Mdhamini wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Pemba, Hamad Ahmed Baucha,
anasema kwa mara ya mwisho aliwafanyia wafanyakazi wake uchunguuzi wa afya zao,
mwaka 2016, na bajeti yake aliitoa kupitia mfuko wa barabara.
“Sisi
mwaka 2013, tuliwafanyia lakini na mwaka jana 2016 pia tuliwafanyia, ingawa
wengine hupuuza tangaazo la kuwafanyia, lakini wengine hasa wanaofanyakazi
kwenye mavumbi hulifurahia”,anabainisha.
Anakiri
kuwa, kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018 kifungu hicho cha fedha hakikuingizwa, ingawa
kwenye bajeti ijayo ya mwaka 2018/2019, watahakikisha kunakuwa na kifungu kwa
ajili gharama ya kuwafanyia uchunguuzi wafanyakazi wao.
Khamis
Mohamed Maliki na Asha Mohamed Hilali ambao ni wafanyakazi wa wizara hiyo,
wamekiri kufanyiwa uchunguuzi wa kiafya, bila ya malipo, ingawa sasa ni mwaka
wa pili hawajafanyiwa tena.
“Mimi
niligundulika na na tatizo la uoni hafifu, na kisha wizara yangu ikanipatiwa
miwani na hadi sasa natumia miwani ambayo gharama ilitoka wizarani
kwangu”,anafafanua.
Afisa
Utumishi wizara ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Pemba,
Mohamed Juma Rashid anasema wao kila mwaka huwafanyia uchunguuzi wafanyakazi
wao wote 110, na wapo waliowagundua na maradhi kadhaa.
“Tulipokwishawagundua
sasa faida yetu kubwa, wanapotuaga kwamba hawahudhurii kazini, tumeshajua
wanakabiliwa na maradhi gani”,anabainisha.
Raya
Ahmada wa wizara hiyo, anasema utekelezaji huo wa sheria ya Afya na Usalama
Kazini no 8 ya mwaka 2005, ya wao kufanyiwa uchunguuzi, haupaswi kudharauwaliwa
na wafanyakazi na hasa wale wanaofanyakazi sehemu za mionzi au vumbi.
Hata
Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba, Bakari Ali Bakar anasema tokea ateuliwe
kushika nafasi hiyo mwaka 2016, hadi sasa hajawahi kuwafanyia uchunguuzi
wafanyakazi wake, na sio kwa sababu ya ukosefu wa bajeti.
“Mimi
tokea nishike nafasi hii mwaka wa pili sasa, sijawahi kuwafanyia uchunguuzi wa
kiafya wafanyakazi wangu 1,257, na hii inatokana na hatujajipanga sisi wenyewe
tu ndani ya ofisi yetu”,anabainisha.
Katibu
Mkuu wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Zanzibar ZATUC Khamis Mwinyi, anasema
wamekuwa wakilifuatili hilo na mengine, ingawa huelezwa kuna uhaba wa vitendea
kazi kwenye kitengo cha afya na usalama kazini.
“Sisi
ZATUC bado tunaiomba serikali kuhakikisha wanaitekeleza sheria hiyo halali, ili
kuona wanawabaini wafanyakazi wanaohitaji kufanyiwa matibabu, ili wafanye kazi
zao kwa ufanisi”,alieleza.
Alibainisha
kuwa mfanyakazi, imara na mwenye uzalisha bora ni yule mwenye afya njema, iwe
kwa kujifanyia uchunguuzi kwa gharama zake, au muajiri kama sheria no 8 ya
mwaka 2005 ya afya na usalama kazini inavyoataka.
Waziri
wa Nchi Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Zanzibar Mhe: Haroun Ali Suleiman, anasema ni wajibu kwa waajiri kuwafanyia uchunguuzi
wa kiafya waajiriwa wao, kama alivyowahi kuwafanyia yeye.
“Japo
kila baada ya miaka miwili, wanatakiwa wawafanyie uchunguuzi, wasiweke umuhimu
na umakini wanapotaka kuwaajiri tu, hiyo sio halali”,alieleza.
Ali
Makame Ali (76) aliekuwa mfanyakazi Kilimo kitengo cha Utibabu wa mimea tokea
mwaka 1964 hadi alipostaafu mwaka 2008, hakumbuki hata siku moja kufanyiwa
uchunguzi wa kiafya hadi anastaafu.
“Likizo
nilikwenda mara 13, ingawa nimeitumikia serikali miaka 44 mfululizo, tokea
nipoajiriwa mwaka 1964 hadi nilipomaliza utumishi kwenye kitengo cha utibabu wa
mimea”,alinieleza.
Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa sasa iko katika mchakato wa mwisho kuhakikisha
wafanyakazi wake wote kwenye sekta za umma wanakuwa na Bima za Afya.
Mwisho
No comments:
Post a Comment