Habari za Punde

Rais Dk Shein afuta uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la nyumba

Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu Namba 53 cha Katiba ya Zanzibar ya 1984 na Kifungu 12 (3) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Namba 2 ya mwaka 2011, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, amefuta uteuzi wa MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA NYUMBA NDUGU MOHAMMED HAFIDH RAJAB kuanzia leo tarehe 12 Oktoba, 2017.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO
ZANZIBAR


12 OKTOBA, 2017     

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.