Habari za Punde

Kampuni ya Simu ya Zantel Yawakomboa Wakulima wa Zao la Mwani Zanzibar.

Mratibu wa Mauzo na Masoko wa Zantel-Zanzibar, Ndg. Haji Said Khatibu (katikati) akimsaidia Mkazi wa kijiji cha Uroa, Mkoani Kusini-Unguja, Bi. Fatma Abbas kuvuna zao la mwani baada ya Kampuni ya Zantel kuwatembelea baadhi ya wakulima walionufaika na msaada wa Tsh milioni 10 zilizotolewa mwaka jana kwa ajili ya kuwaendeleza wakulima hao. Kushoto ni mkazi wa mjini Unguja-Zanzibar Issa Yusuf.

Watu wengi waliopo nje ya Zanzibar wanadhani kuwa Unguja na Pemba ni visiwa vyastarehe na mahali pa kupumzika tu. Uzuri wa Zanzibar umekuwa kivutio kwa watalii kutoka nchi mbalimbaliduniani jambo ambalo linaifanya Zanzibarkuimarika kwenye masuala ya Utaliii.
Hata hivyo ukija kwenye masuala ya Kilimo, watu wengi wamekuwa wakiamini kwamba Utalii na kilimo cha karafuu ndio mambo pekee ya kibiashara yanayofanyika visiwani humo.
Kilimo cha zao la ‘MWANI’kimekuwa ni miongoni mwa mazao makubwa ya biasharayanayouzwa nje ya nchi tangu mwanzoni mwa miaka ya 1990.
Shughuli za kilimo cha zao la mwani zilianza Zanzibar mwaka 1989 na zao hilo limewavuta watu wengi kujishugulisha na biashara hiyo licha ya kuwapo kwa changamotokadhaa wanazokabiliana nazo.
Takribani asilimia 80 ya wanawake Zanzibar wanajishughulisha na kilimo cha zao hilo na wamekuwa wakitoa wito kwa Serikali na Taasisi za watu binafsi kuwasaidia katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Juni mwaka 2016, kampuni ya mawasiliano inayoongoza katika huduma ya intaneti ya Zantel ilikubali kushirikiana na wakulima baada ya kutoa msaada wa shilingi milioni 10 kwa Jumuiya ya Wakulima wa Mwani Zanzibar (JUWAMWANZA) ili kuwawezesha wanachama hao kununua vifaa vya kilimo hicho ikiwamo kamba navijiti (pegs) ambavyo vilisambazwa kwa wakulima wa mwani katika vijiji 83 vilivyopokatika mwambao wa pwani ya Unguja, jambo lililofanikisha kilimo cha zao hilo kuendelea kufanya vizuri.
Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohamed Baucha alisema Kampuni hiyo ya Mawasiliano imefurahishwa kupata mrejesho kuwa msaada walioutoa umeleta mafanikio kwa wakulima wa mwani na kuwaahidi kuendelea kushirikiana na wakulima hao ili kuwasaidia kufanya kilimo cha kisasa na kuongeza uzalishaji zaidi.
Katika mahojiano ya hivi karibuni mjini Zanzibar, Baucha alisema, “Mwaka huu Zantel inasherehekea miaka miwili tangu Millicom ilipoichukua kutoka kwa Kampuni ya Etisalat ya Falme za Nchi za Kiarabu (UAE). Hivyo msaada wetu wa mwaka jana ulikuwa chini ya mradi wa wetu wa Uwajibikaji kwa jamii katika maeneo ambayo tunafanya shughuli zetu na hivyo tuliamua kuwasaidia wanawake ambao wawamejikita kwenye kilimo cha zao la mwani kisiwani hapa.”
Baucha alisema chini ya Millicom, miradi ya Zantel inayosimamiwa na Idara ya Uwajibikaji kwa jamii imejikita kuwasaidia wajasiriamali, makundi maalumu kama vile walemavu, vijana, pia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano sambamba na kuwainua wanawake katika kuleta maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla.
Alisema Zantel kuwasaidia wakulima wa zao la mwani, pamoja na kuitikia wito wa serikali baada ya kuziomba sekta binafsi kuunga mkono juhudi za wakulima 23,354 wa zao la mwani Zanzibar kuhakikisha kwamba wanauza mazao yao na kuongezea thamani.
Kiongozi huyo wa Zantel Zanzibar aliongeza kwamba kampuni hiyo ipotayari kuwasaidia wakulima wa mwani katika nyanja ya mafunzo ili kuwa na ujuzi zaidi kwa kilimo cha kisasa kwa kutumia intaneti ya Zantel kwa kujifunza zaidi kuhusu wakulima wengine wa mwani wa maeneo mengine duniani kujua nini wanachokifanya.
Licha ya kuwapa mafunzo ya jinsi yakutumia intaneti, Zantel itawapa pia elimu ya kutumia huduma ya EzypESA ili kutunza fedha zao na wakati mwingine kuhamisha fedha zao kutoka benki kwenda kwenye mtandao wa Zantel au kwenda kwenye akaunti zao za benki pindi wanapovuna na kuuza mazao yao.
“Tunataka kuwarahishia maisha na kufanyaia wepesi kwa kuhakikisha wanapata  muda mwingi zaidi kwenye kazi zao za uzalishaji wa zao hilo ili waweze kuongeza mauzo badala ya kutumia muda mwingi kwenda mjini kufanya miamala au kukaa kwenye foleni kwa muda mrefu wakisubiri kulipia malipo ya huduma mbalimbali,” aliongeza.
Chini ya umoja wao wa Jumuiya ya Wakulima wa Mwani Zanzibar, imekuwa rahisi kwa Zantel kuwasaidia jambo ambalo wanakiri kwamba limekuwa na manufaa kwao.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa JUWAMWAZA, Pavu Mcha Khamis alisema, “Msaada wa Zantel daima utakumbukwa kutokana na kusaidia vijiji 48 Unguja na maeneo mengine ya Kisiwa cha Pemba.
Alisema wakulima wa mwani wanahitaji vifaa mbalimbali hivyo wanaendelea kutoa wa witokwa Serikali na wadau wengine wanaoitakia mema sekta hiyo kuendelea kuwasaidia wakulima wa zao la mwani.
Pavu alifafanua kwamba wakulima wengi ambao wameelekeza nguvu zao kwenye kilimo cha mwani wanakabiliwa na kutokuwa na ujuzi kwenye kazi hiyo, uhaba wa vifaa ikiwamo viatu vya mpira, Kamba, vijiti na bei ndogo ya zao hilo sokoni vitu ambavyo viliisukumaKampuni ya Zantel kuwa mstari wa mbele katika kutatua baadhi ya changamoto hizo  kwa kushirikiana na wanunuzi pamoja na serikali.
Kwa mujibu wa Pavu, Mwani aina ya Cottoni na Spinosum ndivyo vinastawi kwa wingi Zanzibar na kuna takribani makampuni saba ambayo hununua mwani kutoka kwa wakulima kisiwani humo lakini zaidi Makampuni hayo hununua Spinosum ambayo ndiyo huwa inauzwa pia nje ya nchi.
Alisema kwa kawaida mwani aina ya spinosum huchukua takriban siku 45 na 60 kukua hadi kuvuna na ndio unapatikana kwa wingi kwa sababu mwani aina ya Cottonii unauzwa bei ghali na wakati mwingine mwani huo hukabiliwa na hali mbaya ya mabadiliko ya hewa.
Katika mahojiano ya hivi karibuni na wakulima wa mwani wakielezea jinsi ambavyo wamenufaika na shilingi 10 milioni zilizotolewa na Zantel, Mjane Sharifa Thabit (51)  wa Kijiji cha Pongwe kilichopo, kilometa 43 toka Unguja Kusini,  amekuwa akilima zao hilo tangu lianze kulimwa Zanzibar zaidi ya mongoni mitatu iliyopita, alieleza jinsi ambavyo amefanikiwa kwenye kilimo hicho.
Alisema kwamba vifaa vya kilimo ambavyo vilitolewa na ZantelJuni mwaka jana, vimekuwa msaada mkubwa kwenye shughuli hiyo ya kilimo.
“Tunaishukuru Zantel kwa msaada wao na tunawaomba waendelee kutusaidia. Mipango yetu ni kupata mafunzo kuhusu kilimo cha kisasa cha mwani,” alisema.
Mkulima mwingine wa kijiji cha jirani cha Uroa ambaye anafanya shughuli ya kilimo kama hicho, Fatma Abbasi anasema huwa anavuna mazao yake na kwenda kuyakaushia nyumbani.
“Hii kazi ni ngumu sana lakini tunahitajika kuifanya ili kuendesha maisha,” alisema
Alipoulizwa ni kwa namna gani alinufaika na Shilingi milioni 10 zilizotolewa na Zantel, Alisema “ Ninashukuru sana kuwa sehemu ya watu walionufaika na msaada ule mwaka jana. Imenisaidia sana kutuinua sisi wakulima.”
Alisema baada ya msaada huo wakulima wengi waliweza kuongeza kipato chao jambo lililowawezesha kuongeza uzalishaji na kwa upande wake alifanikiwa kujipatia kati ya shilingi 300,000 na 400,000 wakati wa mavuno ya kwanza.
Pongwe na Uroa ndio vijiji vyenye idadi kubwa zaidi ya watu wanaojishughulisha na kilimo cha mwani katika maeneo ya Visiwa vya Unguja na Pemba lakini bado wamekuwa wakikabiliwa na changamoto za vifaa vya kilimo na bei ndogo yazao hilo.
Zanzibar huuza takriban tani 12,000 za mwani nje ya nchi kila mwaka ikiwa ni ya tatu kwa uuzaji wa mwani duniani ikiwa nyuma ya Phillipines inayoongoza naIndonesia.Zanzibar imeendelea kupata changamoto kubwa ya Soko kutokana na ushindani kutoka kwenye nchi kama Philippines.
Kwa mujibu wa wakulima wanaweza kuzalisha bidhaa zaidi ya 50 kutokana na zao la mwani ikiwamo juisi, dawa za hospitali, vipodozi na vingine vingi zaidi huku nchi za nje wakitumia mwani kama mbolea.
Maeneo mengi ambako hutumia zao hilo kama chakula ni barani Asia  hasa nchi za Japani, Korea na China ambako kilimo cha mwani kimekuwa muhimu katika kuinua Uchumi wa viwanda.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.