Naibu Waziri Mambo yaNdaniyaNchi, Mhandisi Hamad
Masauni,akizungumza na wananchi wanaofanya shughuli zao katika Mpaka wa Tanzania na
Kenya Sirari,
wakati wa ziara ya kikazi aliombatana na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania ,Dkt. Anna
Makakala (wa tatu kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo.Lengo
la ziara hiyo ni kukagua shughuli mbali mbali zilizopo chini ya Idara za Wizara na kukagua mipaka iliyopo katika mkoa huo.
MkuuwaMkoawa Mara, Adam Malima,
akijibu baadhi ya hoja zilizoulizwa na wananchi wanaofanya shughuli zao katika Mpaka wa
Tanzania na Kenya Sirari,wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri Mambo
ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni (wa pili kulia),akiambatana Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dkt.
Anna Makakala (kulia)
Naibu Waziri Mambo yaNdaniyaNchi, Mhandisi Hamad
Masauni,Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala (wa pili kulia),Mkuu wa Mkoa wa
Mara, Adam Malima na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorius Luoga (kulia),wakimsikiliza mmoja wa wananchi wanaofanya shughuli karibu na kituo
cha Mpaka wa Tanzania na Kenya Sirari ,wakati wa ziara ya kikazi yenye lengo
la kukagua mipaka iliyopo ndani ya mkoa huo
Naibu Waziri Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni,Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna
Makakala (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima (wa tatu kulia) wakisikiliza maswali ya mmoja wa wananchi wanaofanya shughuli karibu na kituo
cha Mpaka Tanzania na Kenya Sirari ,wakati wa ziara ya kikazi yenye lengo
la kukagua mipaka iliyopo ndani ya mkoa huo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Na
Abubakari Akida-WMNN
NAIBU Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni, amewataka
wananchi na wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao karibu na Kituo cha Mpaka
wa Sirari unaotenganisha nchi za Tanzania na Kenya kuhakikisha wanashirikiana
na Jeshi la Polisi mkoani Mara kudhibiti matukio ya uhalifu kwa kutoa taarifa
za wahalifu hao kwa jeshi hilo.
Hayo ameyasema akiongea na wananchi wakati wa ziara ya kikazi katika mkoa wa Mara, ikiwa na lengo la kutembelea mipaka iliyopo katika mkoa huo inayotenganisha nchi ya Tanzania na nchi jirani za Kenya na Uganda ambapo katika ziara hiyo aliongozana na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala,Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uzalishaji Vitambulisho vya Taifa,Alphonce Malibiche na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama.
“Tumekuwa tukipata taarifa wananchi wa hapa kushirikiana na wahalifu katika kupitisha mali za magendo hapa hasa wakitumia vijana wanaoendesha bodaboda kupitisha mizigo yao na kuripotiwa matukio mbalimbali yanayohatarisha usalama wa raia wetu,natoa wito kwa wananchi wa hapa kushirkiana na jeshi la polisi kudhibiti matendo hayo ya kihalifu,” alisema Masauni
Aidha,Naibu Waziri Masauni amewataka wananchi hao kuacha mara moja tabia inayokua kwa kasi katika eneo hilo ya kulizuia Jeshi la Polisi kufanya shughuli zake na endapo atabainika mtu yoyote atakumbana na mkono wa sheria huku akitoa ushauri kwa jeshi kuzifanyia utafiti taarifa zitakazoletwa ili kuepuka kumuonea mtu.
Akizungumzana wananchi hao Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dk. Anna Makakala, amewataka wananchi hao kupeleka taarifa za wahamiaji haramu pindi watakapowagundua ili kuweza kudhibiti tatizo la wahamiaji hao kuingia nchini huku akiweka wazi viwango vya udhibiti vilivyoweka na idara yake kuzuia wahamiaji haramu kuingia nchini.
“Idara ya Uhamiaji kupitia wawakilishi wetu mkoani hapa tupo tayari na tunaomba mtu yoyote mwenye taarifa za wahamiaji haramu azifikishe kwenye ofisi ya uhamiaji nasi tutazifanyia kazi kwani tushapunguza tatizo hilo na tuko katika jitihada za kulimaliza kabisa,” alisema Dk. Makakala
Akizungumza kwa niaba
ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taida (NIDA), Kaimu
Mkurugenzi Idara ya Uzalishaji Vitambulisho vya Taifa, Alphonce Malibiche,
alisema NIDA imezindua zoezi la usajili wa vitambulisho kwa wakazi wa Mkoa wa
Mara na wanatarajia kumaliza zoezi hilo mapema ili wananchi wa Mkoa huo na
wilaya zake wawe na vitambulisho vya Taifa vitakavyozuia baadhi ya changamoto
lakini lengo kubwa ni kuhakikisha kila Mtanzania anakua na Kitambulisho cha
Taifa.
No comments:
Post a Comment