Na Mwandishi wetu
Wachezaji wa Timu ya Taifa
ya Kenya Harambee Stars wameahidiwa kila mchezaji kupewa kiasi cha Laki mbili
za Kenya ambazo ni sawa na Sh Milioni 4 kwa kila mchezaji endapo itaibuka
washindi dhidi ya Zanzibar Heroes katika mchezo wa fainali unaotarajiwa klufanyika
kesho katika Uwanja wa Kenyatta mjini Machakos nchini Kenya.
Chama cha Mpira cha Kenya, Football Kenya Federation kimetoa ahadi hiyo kupitia mwenyekiti wake Nick
Mwenda alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huku akisema wametenga
kiasi cha Sh Milioni sita za Kikenya kwa ajili ya zawadi kwa wachezaji pamoja
na benchi la ufundi
Wakati huo huo magazeti ya
Kenya katika kuonesha kuingiwa na kiwewe na woga kuikabili Zanzibar Heroes
wameanza kuingiza Imani za kichawi na kishirikana baada ya kuwashuku Zanzibar
kwamba kila kila wakianza mpira mwanzo wa mchezo basi pasi yao ya pili lazima
ipigwe nje ya uwanja kwa mujibu wa kamati yao ya ufundi ilivyowaagiza
Hata hivyo kiungo mahiri wa
Zanzibar Heroes, Mchezaji wa Mtibwa Sugar, Mohammed Issa 'Banka' amepuuzia
habari hizi na kusema ni ari na umoja wa timu ndio vitu pekee vilivyowasaidia
kwani kwa Zanzibar Heroes kucheza michezo ya CECAFA ni kama kupanda ndege
kwenda Urusi kucheza Kombe la Dunia.
Banka alizidi kusisitiza: ‘Zanzibar
ni nchi ndogo sana na wengi wetu ni maskini hivyo CECAFA kwetu ni kama World
Cup hivyo ni sehemu pekee kwetu kucheza kwa kiwango cha hali ya juu si uchawi jamani’
Alimalizia Mohammed Issa ‘Banka’
Tayari Baraza la Wawakilishi limetoa ahadi ya kuwazawadia Zanzibar Heroes Sh Milioni kumi na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed akisistiza ahadi yake ya kuwapongeza na kuwazawadia Heroes ipo palepale.
Akizungumza na Waandishi wa habari kwa niaba ya Rais wa Zanzibar Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma amesema kutokana na hatua iliyofikia timu hiyo kwa jitihada waliyoiyonesha vijana hao katika michuano hiyo Dk. Shein chini ya serikali yake ameahidi kuwapa zawadi vijana wa Zanzibar Heroes pindi watakapo rejea Zanzibar.
Akizungumza na Waandishi wa habari kwa niaba ya Rais wa Zanzibar Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma amesema kutokana na hatua iliyofikia timu hiyo kwa jitihada waliyoiyonesha vijana hao katika michuano hiyo Dk. Shein chini ya serikali yake ameahidi kuwapa zawadi vijana wa Zanzibar Heroes pindi watakapo rejea Zanzibar.
No comments:
Post a Comment