Habari za Punde

Straika Kassim Suleiman Khamis kukosa michezo iliyosalia Cecafa



Na Abubakar Khatib Kisandu, Machakos Kenya.

Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes), Kassim Suleiman Khamis anatarajiwa kukosa michezo yote iliyosalia katika Mashindano ya Cecafa Senior Chalenj Cup yanayoendelea nchini Kenya.

Mshambuliaji huyo anaecheza klabu ya Tanzania Prisons kwenye ligi kuu soka Tanzania Bara ameumia mguu  wake wa kulia baada ya kugongana na Daniel Lyanga wa Kilimanjaro Stars katika mchezo ambao Zanzibar Heroes walipoichapa Tanzania Bara mabao 2-1.

Daktari Mkuu wa Zanzibar Heroes, Mohd Said alithibitisha taarifa hizo za kukosa huduma ya mshambuliaji huyo.


“Awali tulitegemea angeweza kuipata nusu fainali na mchezo wa mwisho, lakini mpaka sasa dalili hiyo haipo tena na atalazimika kukosa mashindano yote haya ukiwemo mchezo wa kesho dhidi ya Uganda na ule wa mwisho”. 

Kassim ndie kinara wa kufunga mabao kwa upande wa Zanzibar baada ya kufunga mabao mawili yote akitokea benchi katika michezo Heroes iliposhinda 3-1 dhidi ya Rwanda na ule wa 2-1 dhidi ya Tanzania bara na kupelekea vilabu vingi ikiwemo Simba kuhitaji huduma yake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.