Mkurugenzi Mkuu wa Zantel,
Sherif El-Barbary akizungumza na vyombo vya habari hivi karibuni mjini Zanzibar
wakati wa hafla ya utiaji saini kati ya Zantel na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB)
ikiwa ni ushirikiano wa kurahisisha huduma ya ulipaji kodi kwa njia ya simu
kupitia huduma ya EzyPesa kutoka Zantel. Kushoto ni Mkuu Zantel kisiwani
Zanzibar, Mohamed Mussa Baucha.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Sherif El-Barbary (kulia) na Kamishna wa
Bodi ya Mapato Zanzibar, Ndugu Amour Hamil Bakari (Aliyekaa katikati) wakitia
saini ya makubaliano ya kushirikiana katika kurahisisha huduma ya ulipaji kodi
kwa njia ya simu kupitia huduma ya EzyPesa hivi karibuni mjini Zanzibar.
Anayeshuhudia kulia ni Makamu wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Bi. Khadija
Shamte Mzee.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Sherif El-Barbary (kulia) na Kamishna wa
Bodi ya Mapato Zanzibar, Ndugu Amour Hamil Bakari (Aliyekaa katikati) wakitia
saini ya makubaliano ya kushirikiana katika kurahisisha huduma ya ulipaji kodi
kwa njia ya simu kupitia huduma ya EzyPesa hivi karibuni mjini Zanzibar.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Sherif El-Barbary (wa pili kushoto) na
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Ndugu Amour Hamil Bakari (wa pili kulia) wakipeana
mkono huku wakishuhudiwa na Makamu wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Bi. Khadija
Shamte Mzee (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Mikakati na Utendaji wa biashara
Zantel, Shinuna Kassim baada ya kutiliana saini ya makubaliano na ushirikiano
katika kurahisisha huduma ya ulipaji kodi kwa njia ya simu kupitia huduma ya
EzyPesa. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni mjini Zanzibar.
Zantel kwa kushirikiana
na Bodi ya Mamlaka ya Mapato ya Zanzibar wameingia katika makubaliano ambayo
yatawawezesha wakazi wa kisiwani hapa kurahisisha huduma ya ulipaji kodi kwa
njia ya simu kupitia huduma ya EzyPesa inayotolewa na Kampuni ya Mawasiliano ya
Zantel.
Ushirikiano huo unawezesha wateja wote wa Bodi ya Mapato
Zanzibar kuweza kufanya miamala ya malipo ya kodi bila usumbufu wowote kupitia
EzyPesa.
Hii inamaanisha kwamba walipa kodi wa ndani wataweza kulipa
kodi zao husika ikiwamo ushuru wa forodha na kodi zingine kama PAYE na VAT kwenye
uingizaji wa biadhaa kupitia mfumo wa EzyPESA.
Akizungumza wakati wa hafla ya kutiliana saini ya makubaliano
hayo Alhamisi ya tarehe 14 Desemba 2017, Mkurugenzi Mtendaji wa Zantel, Sherif
El Barbary akiwa ameambatana na Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Amour
Hamil Bakari na Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohamed Mussa (Baucha) alisema lengo
kuu la huduma hiyo ni kuwawezesha wakazi wa Zanzibar kulipa kodi kwa urahisi
zaidi kupitia huduma ya EzyPesa ya Zantel.
Alisema kuwa hatua hiyo ya makubaliano inaendana sawa na dira
ya Bodi ya Mapato Zanzibar, yenye lengo la kuwa kitovu cha ukusanyaji mapato
chenye ufanisi, jambo ambalo litaiwezesha
nchi kuongeza pato la taifa la ndani kwa mwaka (GDP).
“Kama tunaweza kuongeza ukusanyaji wa mapato kupitia huduma
ya EzyPesa na pato la Taifa GDP litaongezeka zaidi. Hii itasaidia kuimarisha
uchimi wa Taifa zima, na kwa namna nyingine kipato cha mwananchi wa kawaida
kitaongezeka.
Alisema Zantel ni miongoni mwa kampuni inayoongoza katika
kuchangia malipo makubwa ya kodi kwa Serikali ya Zanzibar na mtandao huo
utaendelea kuhakikisha unaendelea na utaratibu wa kusaidia Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Bodi ya
Mapato ya Zanzibar ili kuhakikisha kwamba
wanakusanya kodi kwa kadri wanavyoweza kupitia huduma ya EzyPesa.
Takwimu zinaonyesha kwamba Zantel inalipa Shilingi blioni 2
kama kodi kwa serikali ya Zanzibar kila mwezi ambapo ni takribani shilingi 24
bilioni kwa mwaka.
“Lengo la ushirikiano huu ni kuhakikisha tunawasogezea wananchi
huduma za ulipaji kodi karibu na maeneo yao, nikimaanisha kuwa sasa
hawatohitaji kupoteza muda mwingi kuzifuata huduma za kodi ofisini kwetu bali
zitakuwepo viganjani mwao,” alisema Kamishna wa Kodi wa Bodi ya Mapato
Zanzibar, Amour Hamil Bakari.
Alisema lengo kuu la Bodi ya Mapato Zanzibar ni kusogeza huduma
karibu kwa wateja wake, kuimarisha shughuli za utendaji wa kila siku za taasisi
hyo ikiwa ni pamoja na kubuni mbinu mbadala za kuongeza ukusanyaji wa mapato
Zanzibar.
KWA MAELEZO ZAIDI:
Rukia Mtingwa
Baruapepe:
r.mtingwa@zantel.co.tz
No comments:
Post a Comment