Habari za Punde

SERIKALI YA JAPAN YAAHIDI KUENDELEA KUSAIDIA MIRADI YA UMWAGILIAJI NCHINI


Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaharu Yoshida  akiweka jiwe la msingi shamba la mafunzo ya Uandisi,Ujenzi na Umwagiliaji la Oljoro wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha linalotumiwa na wanafunzi wa fani hiyo wa Chuo cha Ufundi Arusha(ATC),kushoto ni Kaimu Mkuu wa chuo hicho,Dk Masudi Senzia.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha(ATC),Dk Masudi Senzia(kushoto) akimshukuru Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaharu Yoshida  baada ya kuweka jiwe la msingi katika shamba la mafunzo ya Uandisi,Ujenzi na Umwagiliaji.


Miundombinu ya umwagiliaji  kwenye shamba lenye ukubwa wa eka 150 litawezesha kupata wahitimu walioiva kivitendo 

Baadhi ya wanachuo wakitoka kwenye darasa la mafunzo kwa vitendo.

Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaharu Yoshida(katikati) akifatiwa nyuma na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha(ATC),Dk Masudi Senzia kukagua bwawa linalotumika kwaajili ya kukinga maji ya mvua na kuyatawanya kwenye mashamba ya mafunzo.
Mkurungezi wa Elimu ya Ufundi nchini,Mhandisi Thomas Katebelirwe akizungumza katika halfa hiyo.

Makamu Mkuu wa Chuo cha ATC anayeshughulikia Utawala,Fedha na Mipango,Dk Erick Mgaya akizungumza umuhimu wa shamba hilo ambalo litasaidia kuwapata wataalamu waliobobea nchini katika fani ya umwagiliaji.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.