Habari za Punde

Dkt MWINUKA atembelea Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme, IBADAKULI

Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito Mwinuka, ametembelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.
Katika ziara hiyo, Dkt. Mwinuka amejionea shughuli mbalimbali zinazofanyika kituoni hapo.
Kituo hicho ni mojawapo ya vituo vilivyofanyiwa upanuzi wakati wa utekelezaji wa Mradi wa njia ya Kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 (Backbone) kutoka Mkoani Iringa hadi Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito Mwinuka, akisaini Kitabu cha Kumbukumbu ya Wageni Wakati alipotembelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.
Muonekano wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.