VIONGOZI mbali mbali wa Serikali wakiongozwa na
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili, Mohamed Aboud Mohamed watatu kutoka
kulia, wapili Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othaman na wakanza ni
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Hemed Suleiman Abdalla, wakimsubiri kumpokea
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Sluhu Hassan.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Karume,Pemba. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Karume,Pemba. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mshauri wa Rais wa Zanzibar Pemba Dkt. Maua Daftari mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Karume,Pemba. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
ASKARI wa JWTZ Kisiwani Pemba wakiwa katika mstari
mmoja, kwa lengo la kutoa heshima zao kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Samia Sluhu Hassan mara wakati atakapowasili katika kaburi la
Marehemu Dr Omar Ali Juma lililopo Ditia Wawi Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Samia Sluhu Hassan, akisalimiana na mmoja wa askari wa JWTZ baada ya baada ya
kuwasili katika kaburi la Dr Omar Ali Juma, kwa lengo la kuweka shada la maua
katika ziara ya siku tatu kisiwani humo.(PICHA
NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Mhe:Samia Sluhu Hassan, akipokea shada la mauwa kutoka kwa mmoja wa askari wa
JWTZ Kisiwani Pemba, kwa ajili ya kuweka katika kaburi la Marehemu Dr Omar Ali
Juma aliyefariki dunia Julai 4/2001 na kuzikwa Ditia Wawi Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Mhe:Samia Sulhu Hassan, akiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Dr Omar
Ali Juma lililopo Ditia Wawi Wilaya ya Chake Chake, baada ya kuwasili Kisiwani
Pemba kwa ziara ya Siku tatu.(PICHA NA
ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe:Samia Sluhu Hassan, akitoa heshima katika kaburi la Marehemu Dr Omar Ali
Juma, aliyefariki dunia Julai 4/2001 na kuzikwa kijijini kwao Ditia Wawi Wilaya
ya Chake Chake, mara baada ya kuwasili Kisiwani Pemba kwa ziara ya Siku tatu.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia
Sluhu Hassan, akiweka saini katika moja ya vitabu baada ya kuwasili katika
kaburi la marehemu Dr Omar Ali Juma, lililopo Ditia Wawi Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
VIONGOZI mbali mbali wa SMT na SMZ, wakanza kushoto
ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Shaaban Seif Mohamed, katikati
Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Injinia Hamad Yussuf Masauni, watatu ni Mkuu wa
Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman Abdalla.(PICHA
NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Samia Sluhu Hassan, akisikiliza kwa makini dua mbali mbali zilizotolewa kwa
ajili ya kumuombe Marehemu Dr Omar Ali Juma, baada ya kuwasili katika kaburi
lake Ditia Wawi Wilaya ya Chake Chake.(PICHA
NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
No comments:
Post a Comment