Na Yusuph Mussa, Korogwe
IMMAMATUKIO BLOG
Choo hiki cha darasa la awali kijiji cha Lwengera- Relini kina miaka saba ujenzi wake haujakamilika, hivyo kufanya watoto waliokuwa wanasoma hapo kuhamishwa kijiji kingine Lwengera- Darajani. Chatanda ametoa sh. 500,000 ili kukamilisha choo hicho na watoto warudishwe kusoma hapo, ambapo itawapunguzia usumbufu wa kutembea kilomita tatu Shule ya Msingi Lwengera- Darajani, kwenda na kurudi.
Kutokana na darasa la awali katika Shule ya Msingi Lwengera- Relini kufungwa kwa kukosa choo, limeanza kutoa nyufa na kuharibiwa rangi na mchwa. Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini Mary Chatanda ametoa sh. 500,000 ili kukamilisha choo hicho, huku akiitaka Halmashauri ya Mji Korogwe kukarabati jengo hilo.
Jengo la Darasa la Awali Kijiji cha Lwengera- Relini celling board zake zikiwa zimeachia kutokana na kushindwa kutumika. Ni baada ya watoto waliokuwa wanasoma hapo kuhamishwa kwa kukosa choo.
On Thursday, March 1, 2018, 1:12:41 PM GMT+3, khalfan said
MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Mjini mkoani Tanga (CCM) Mary Chatanda ameshangazwa kuona darasa la awali katika Kijiji cha Lwengera- Relini, Kata ya Old Korogwe katika Halmashauri ya Mji Korogwe limekaa miaka saba bila choo.
Matokeo yake, darasa hilo limefungwa na watoto waliokuwa wanasoma hapo imebidi wahamishiwe Shule ya Msingi Lwengera- Darajani na kulazimika kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita sita kila siku kwenda shuleni.
Chatanda ambaye alifika leo Machi mosi, 2018 kukagua shughuli za maendeleo kwenye kijiji hicho, alisema sababu ya Serikali kujenga darasa hilo la awali, ni kuwapunguzia mwenda wa kutembea watoto wa kijiji hicho ambao walikuwa wanalazimika kwenda shule ya msingi kijiji cha jirani cha Lwengera- Darajani.
"Serikali ilikuwa na makusudi kwa kujenga darasa hili, nia ni kuwapunguzia umbali wa kutembea kwenda Lwengera- Darajani, lakini darasa hili miaka sabaMatokeo yake, darasa hilo limefungwa na watoto waliokuwa wanasoma hapo imebidi wahamishiwe Shule ya Msingi Lwengera- Darajani na kulazimika kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita sita kila siku kwenda shuleni.
Chatanda ambaye alifika leo Machi mosi, 2018 kukagua shughuli za maendeleo kwenye kijiji hicho, alisema sababu ya Serikali kujenga darasa hilo la awali, ni kuwapunguzia mwenda wa kutembea watoto wa kijiji hicho ambao walikuwa wanalazimika kwenda shule ya msingi kijiji cha jirani cha Lwengera- Darajani.
Choo hiki cha darasa la awali kijiji cha Lwengera- Relini kina miaka saba ujenzi wake haujakamilika, hivyo kufanya watoto waliokuwa wanasoma hapo kuhamishwa kijiji kingine Lwengera- Darajani. Chatanda ametoa sh. 500,000 ili kukamilisha choo hicho na watoto warudishwe kusoma hapo, ambapo itawapunguzia usumbufu wa kutembea kilomita tatu Shule ya Msingi Lwengera- Darajani, kwenda na kurudi.
Kutokana na darasa la awali katika Shule ya Msingi Lwengera- Relini kufungwa kwa kukosa choo, limeanza kutoa nyufa na kuharibiwa rangi na mchwa. Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini Mary Chatanda ametoa sh. 500,000 ili kukamilisha choo hicho, huku akiitaka Halmashauri ya Mji Korogwe kukarabati jengo hilo.
Jengo la Darasa la Awali Kijiji cha Lwengera- Relini celling board zake zikiwa zimeachia kutokana na kushindwa kutumika. Ni baada ya watoto waliokuwa wanasoma hapo kuhamishwa kwa kukosa choo.
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOSHI
SERIKALI ya awamu ya tano
imedhamiria kwa dhati kuhakikisha wafanyakazi wanalindwa na kupata haki zao
pindi wanapopatwa na madhara yatokanayo na kazi, Naibu Waziri Ofisi ya
Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde
amesema mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro..
Mheshimiwa
Mavunde ameyasema hayo jana (Machi 1, 2018), wakati akiendelea na ziara yake ya
kushtukiza ili kuwabaini waajiri ambao bado hawajatekeelza takwa la kisheria
linalowataka waajiri wote katika sekta rasmi,(umma na binafsi), waliopo
Tanzania Bara kujisajili na kuchangia kwenye Mfuko huo.
Kwa mujibu wa Sheria
iliyoanzisha Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, Ikiwa Mwajiri hatajisajili kwenye
Mfuko, atakuwa ametenda kosa la jinai kwa mujibu wa kifungu cha 71(4) cha
Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi na akipatikana na hatia adhabu yake ni kulipa
faini isiyozidi shilingi milioni 50,000,000 (Milioni Hamsini) au kifungo
kisichozidi miaka mitano jela au adhabu zote kwa pamoja, alisema Mhe. Mavunde.
Mheshimiwa Mavunde
ambaye alifuatana na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko huo Bw. Anslem Peter na
Kaimu Kamishna kutoka Idara ya Kazi, Bi. Rehema Moyo, alibaini Mkoa wa
Kilimanjaro wenye jumla ya Waajiri 1,039 ni waajiri 525 tu ndio wamejisajili
huku wengine 514 bado hawajajisajili na Mfuko.
“Serikali ilikwishatoa
matamko mbalimbali yanayowahimiza waajiri kutekeleza takwa hilo la kisheria, na
leo hii hakuna njia nyingine, Waajiri hawa tuliowabaini hapa Mkoani Kilimanjaro
naagiza WCF iwapeleke mahakamani haraka iwezekanavyo ili sheria ichukue mkondo
wake.” Alisema.
Baadhi ya waajiri ambao
Naibu Waziri na timu yake walifanya ukiaguzi huo ni pamoja na kampuni ya
Machare Investments, Scholastica Schools iliyoko Himo nje kidogo ya mji wa
Moshi.
Alisema sio lengo la
serikali kuwatisha au kuwadhalilisha waajiri hao bali nia ni kuhakikisha haki
za wafanyakazi zinalindwa lakini pia kuwaondolea jukumu waajiri la kuwahudumia
wafanyakazi wao wanapopatwa na madhara wakiwa kazini.
“Tunataka
ninyi wawekezaji, (waajiri), mjielekeze kwenye shughuli zenu za msingi kwa
maana ya kufanya uwekezaji na biashara zenu na hili la kumuhudumia mfanyakazi
aliyepatwa na madhara kazini lishughulikiwe na serikali.” Alisisitiza.
Tayari
Mhe. Mavunde amefanya ziara kama hiyo mkoani Mwanza na Shinyanga na kubainisha
kuwa operesheni hiyo ya kuwabaini waajiri wasiotekeleza takwa hilo la kisheria
litafanyika nchi nzima, na kuwataka waajiri kufanya hivyo haraka ili wasijikute
kwenye matatizo.
“Tumewasambaza
maafisa wetu wa WCF mikoani na wanaednelea na utaratibu wa kuwafuikisha
mahakamani waajiri wote ambao wameshindwa kufuata sheria.
Mhaisbu wa Shule ya Scolastica mjini Moshi, Kilimanjaro Bw. Moshi W. Moshi, na Mkuu wa shule hiyo Bw.Michael Shiloli, wakisikilzia maagizo ya Naibu Waziri Mavunde. |
Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter, (kulia), akijadili jambo na Kaimu Afisa Kazi Mkoa wa Kilimanjaro, Bi.Neema Msyalika na Afsia Mwandamizi wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano WCF, Bw. Sebere Fulgance.
Mhe. Mavunde akizungumza na Mkurugenzi wa Machare Investments, (kulia)
Bw. Anselim Peter akizungujza na waandishi wa habari
Mhe. Mavunde akisisitiza jambo kwa viongozi wa shule ya Scolastica.
Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter, (kulia), akijadili jambo na Kamishna wa kutoka Idara ya Kazi, Bi. Rehema Moyo, (katikati), na Kaimu Afisa Kazi Mkoa wa Kilimanjaro, Bi.Neema Msyalika
No comments:
Post a Comment