Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akiwahutubiwa Wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja Zanzibar wakati wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani Kitaifa imeadhimishwa katika Mkoa huo katika viwanja vya Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein
amesema kuwa Zanzibar bila ya vitendo vya udhalilishaji wa wanawake na watoto inawezekana
iwapo kutakuwa na ushirikiano katika kuvipiga vita vitendo hivyo.
Mama Shein aliyasema hayo leo katika maadhimisho
ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Koba huko
Makunduchi Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja.
Katika maelezo yake Mama Shein alitumia fursa hiyo
kutoa pongezi kwa juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Wajumbe
wa Baraza la Wawakilishi kwa kupambana na vitendo vya udhalilishjaji wa
wanawake na watoto hapa nchini.
Alisema kuwa vitendo vya udhalilishaji wa wanawake
na watotyo vinaendelea akusikika katika jamii, hivyo jamii ni lazima
ishirikiane na Serikali katika kupiga vita vitendo hivyo.
Aliwataka wananchi kutowaonea aibu wala muhali
wahusika kwa kutoa taarifa katika vyombo vya sheria ili wachukuliwe hatua.
Aidha, aalisisitiza jambo la kuzingatia ni kuiwa
mabadiliko yanayosisitizwa katika ujumbe wa mwaka huu yaende sambamba na
mikakati ya Serikali ya kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa wanawake
na watoto kama ilivyoainishwa katika Mpango Kazi wa mwaka 2017 hadi 2022 dhidi
ya vitendo hivyo.
Mama Shein alieleza kuvutiwa sana na ujumbe wa
maadhimisho ya mwaka huu usemao “Wakati umefika: Tushirikiane kuleta mabadiliko
ya wanawake vijijini”.
Alieleza kuwa ni dhahiri kuwa ujumbe huo
umezingatia uhalisia uliopo katika jamii kwamba wanawake wanaoishi vijijini
ndio wanaokabiliwa na changamoto nyingi za kimaendeleo kuliko wale wanaoishi
mjini.
Mama Shein alitoa pongezi maalum kwa uongozi wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Awamu ya Saba chini ya uongozi wa Rais Dk.
Ali Mohamed Shein kwa kuchukua jitihada mbali mbali za kuleta maendeleo ya
Wanawake.
Alieleza kuwa jitihada hizo ni pamoja na
kurekebisha Sera na Sheria ili kuwawezesha wanawake kukabiliana vyema na
changamoto mbali mbali ambazo zilikuwa zikipunguza kasi ya maendeleo ya wanawake
katika masuala mbali mbali katika jamii.
Katika hotuba yake hiyo, Mama Shein aliwataka
wanawake kutumia nafasi zao kuendelea kuhimiza amani na mshikamano kwani mambo
hayo yakitoweka waathirika wakubwa huwa ni wanawake na watoto.
Vile vile aliwataka wanawake kushirikiana katika
malezi bora ya watoto kulingana na maadili, silka na utamaduni wa Kizanzibari
ili watoto wawe raia wema, wazalendo na wenye maadili na hofu ya MwenyeziMungu.
Sambamba na hayo, Mama Shein aliwataka wanawake
kutafakari maendeleo, changamoto na fursa za wanawake katika jamii na
kuwakumbusha wanawake na jamii kwa jumla kuwa wanawake ndio nguzo ya familia.
Hivyo, ni vyema wakatambua kuwa wanawake wana
mchango mkubwa katika kuyatekeleza vyema majukumu yao na kusisitiza kuwa
familia ikiimarika na kupata ustawi ndipo jamii nzima nayo hustawi na kupiga
hatua za maendeleo.
Pia, Mama Shein alieleza kuwa ni vyema wakatambua
kuwa wanawake wana mchango mkubwa katika kuyatekeleza vyema majukumu yao na
kusisitiza kuwa familia ikiimarika na kupata ustawi ndipo jamii nzima nayo
hustawi na kupiga hatua za maendeleo.
Pia, Mama Shein alieleza kuwa wanawake wana
mchango mkubwa katika mapambano dhidi ya UKIMWI na kudhibiti maambukizo ya
Virusi vyake kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto huku akisisitiza kuwa Zanzibar
inaungana na nchi nyengine duniani katika kumaliza maradhi hayo ifikapo mwaka
2030.
Pamoja na hayo, Mama Shein aliwataka wanawake
kupeana moyo na kuzitumia fursa mbali mbali za kujiimarisha kiuchumi, ili
kujiongezea kipato na kupambana na umasikini ikiwa ni pamoja na kujiunga katika
vikundi vya ushirika wa aina mbali mbali ili iwe rahisi kwa Serikali na
washirika wengine wa maendeleo kuwaunga mkono. Mapema Mama Shein alipata fursa
ya kutembelea maonyesho ya vitu mbali mbali yaliyoandaliwa katika maadhimisho
hayo.
Nae Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na
Watoto, Maudline Castiko alieleza juhudi kubwa zinazochukuliwa na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha wanawake wa Zanzibar wanapata haki zao
za msingi huku akisisitiza azma ya Serikali ya kupambana na vitendo vya
udhalilishaji wa wanawake na watoto.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Fatuma Kharib Bilal
alisema kuwa ujumbe wa siku ya wanawake duniani umekuja wakati muwafaka ambapo
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Taasisi husika ikiwemo Wizara hiyo
imekuwa ikichukua juhudi za makusudi katika kuleta mabadiliko kwa wanawake
vijijini pamoja na kuondoa vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Nao “UN Woman” ulipongeza juhudi za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwapa kipaumbele wanawake sambamba na kuwapa haki
zao za msingi huku ukiahidi kuendelea kuiunga mkono Zanzibar.
Mapema akisoma risala ya Wanawake wa Zanzibar,
Zawaadi Akida alieleza kuwa wanawake wa Zanzibar wamefurahishwa sana na
mchakato unaoendelea wa kuhakikisha watendaji wa vitendo vya udhalilishaji wa wanawake
na watoto hawana dhamana na kuzitaka vyombo husika kusimamia kwa makini ili
kuinusuru jamii ya Kizanzibari na matukio hayo.
Alieleza kuwa wanawake wa Zanzibar wanajivunia
mafanikio yaliyopatikana hapa Zanzibar hivi sasa ikiwa ni pamoja na kuwainua
wanawake vijijini kwa kuwapatia na kuwaunganisha na fursa mbali mbali za
maendeleo.
Wanawake hao walieleza kuwa vijiji vingi vya
Zanzibar hivi sasa vimekuwa vikipata huduma mbali mbali muhimu zikiwemo afya,
elimu, maji safi na salama pamoja na fursa za mikopo na taaluma za ujasiriamali
kwa ajili ya kuinua hali za kiuchumi.
Zawadi alieleza kuwa pamoja na maendeleo
yaliopatikana wanawake wa vijijini bado wanakabiliwa na changamoto ambazo
zinarejesha nyuma maendeleo yao miongoni mwake ni ukosefu wa soko la uhakika
kwa bidhaa wanazozizalisha, kukosa fursa za kumiliki rasilimali hususan ardhi
pamoja na udhalilishaji wa wanawake na watoto.
Hafla hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali
akiwemo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Mgeni Hassan, Makamo Mwenyekiti wa
UWT Taifa, Thuwaiba Kisasi na viongozi wengine wa Serikali na Mkoa huo ambapo
Vikundi mbali mbali vya sanaa vilitumbuiza.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment