Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati)alipokuwa akifunga Kongamano la Kitaifa la Utawala Bora na Uchumi Zanzibar lililofanyika jana katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Zanzibar (kulia) Waziri wa Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati, [Picha na Ikulu],16 Machi 2018. 

Waziri asiyekuwa na Wizara maalum Mhe,Said Soud Said akionesha Ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM wakati alipokuwa akitoa mchango wake wakati wa Kongamano la Kitaifa la Utawala Bora na Uchumi Zanzibar lililofanyika jana katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Zanzibar, [Picha na Ikulu],16 Machi 2018.
STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
16.03.2018

RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amewataka viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kuwaeleza wananchi mafanikio makubwa yaliopatikana kutokana na juhudi
za Serikali yao.
Dk. Shein aliyasema hayo
wakati akifunga Semina ya Utawala Bora na Uchumi katika ukumbi wa zamani wa
Baraza la Wawakilishi, Kikwajuni mjini Zanzibar, iliyowashirikisha viongozi wa Wizara
na Taasisi mbali mbali za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Akifunga Semina hiyo, Rais
Dk. Shein alisema kuwa mafanikio yaliopatikana ni makubwa sana hivyo ni vyema
wananchi wakaelezwa kupitia vyombo vya habari, wanasiasa na hata viongozi wa
Taasisi na Wizara za Serikali pia, wanapaswa kuwaeleza wananchi mafanikio hayo.
Alieleza kuwa hatua
iliyofikiwa ni kubwa sana hivyo ni vyema viongozi wakawaambia wananchi kwa kila
ngazi kuazia Shehia, Wilaya, Mikoa na Serikali yote kwa ujumla kuwaeleza
wananchi jinsi Serikali yao ilivyopata mafanikio kwani viongozi hao wana haki
ya kuongea na wananchi sehemu yoyote.
“Kuna mambo mengine tunacchukua
muda mrefu kuwaeleza wananchi hivyo ni
vyema tukatumia mbinu na vyombo vya habari na hata sisi wenyewe kuwaeleza
wananchi mafanikio ya Serikali……kwa vyoyote vile hatua tuliofikia ni nzuri na
tusione tabu kuwaeleza wananchi kwani sisi tunawajika kwao, ndio
waliotuchagua”,alisisitiza Dk. Shein.
Aidha, Dk. Shein aliwaeleza
viongozi hao kuwa uchumi wa Zanzibar uko vizuri, hivyo ni lazima ukaendelezwa
sambamba na kuthamini kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Dk. Shein alisisitiza umuhimu
wa viongozi wote kuwa na nakala za Mipango Mikuu ya Serikali katika ofisi zao
pamoja na kutumia nakala za semina hiyo katika utekelezaji wa majukumu yao ya
kazi kama ni nyenzo muhimu katika kutekeleza majukumu yao.
Alieleza matumaini yake
kwamba mafunzo ya semina hiyo yatakuwa na mchango mkubwa katika kujenga kasi na
hamasa za utendaji kwa viongozi hao pamoja na wale walio chini ya dhamana zao.
Pamoja na hayo, Rais Dk.
Shein alisisitiza kuwa kasi iliyofikiwa katika kuimarisha uchumi wa Zanzibar
tokea mwaka 2010 hadi hivi leo ni kubwa hivyo ni vyema ikaendelezwa na wananchi
wakaelezwa.
Alieleza kuwa viongozi wote
wanawajibika kwa wananchi hivyo ni vyema wakajua kuwa wananchi wanamataraji
makubwa kutoka kwao na si vyema wananchi wakalalamika hatua ambayo inatokana na
kutojua na kutoelezwa mafanikio yaliofikiwa na Serikali yao.
Nae, Waziri wa Ardhi,
Nyumba, Maji na Nishati Salama Aboud Talib ambaye pia, ni Kaimu Waziri wa Fedha
na Mipango akitoa neno la shukurani kwa Rais Dk. Shein, alimpongeza kwa
ushiriki wake katika Semina hiyo ya siku moja ambapo Dk. Shein ndiye aliekuwa
Mwenyekiti wa Semina hiyo.
Waziri Salama alimpongeza
Rais Dk. Shein kwa juhudi zake kubwa za kuhakikisha Zanzibar inapata maendeleo
makubwa ya kiuchumi na kijamii.
Aidha, Waziri huyo
alimuhakikishia Rais Dk. Shein kuwa kila kiongozi aliyeshiriki katika semina
hiyo atalitekeleza agizo lake la kuyafanyia kazi mafunzo waliyoyapata ikiwa ni
pamoja na kwenda kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ili
chama hicho kiendeleze ushindi katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020.
Akitoa mada juu ya “Mwenendo
wa Uchumi wa Zanzibar Kuelekea Mwaka 2020”, Dk. Rahma Salum Mahfoudh alieleza
kuwa katika kipindi hichi cha uongozi wa Serikali ya Awamu ya Saba Zanzibar
imepata mandeleo makubwa katika sekta mbali mbali za kiuchumi na kijamii ambayo
ni matokeo ya utekelezaji mzuri wa Dira ya Maendeleo, MKUZA na Ilani ya
Uchaguzi ya CCM.
Aliwasisitiza viongozi
wote wa Serikali kwa kutumia dhamana zao walizopewa kuendelea na kasi hiyo na
kuimarisha mashirikiano ili kufikia malengo yaliopangwa katika Mipango ya
Maendeleo ambayo mingi ya Mipango hiyo inamalizika katika kipindi cha mwaka
2020.
Hata hivyo, alisisitiza
haja ya kutumia uzoefu uliopatikana katika utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo
katika kipindi kilichopita ili kuweza kukabiliana na changamoto mbali mbali
zinazoweza kujitokeza katika kipindi hiki kiliopo.
Nao viongozi hao
wakichangia mada saba zilizotolewa katika Semina hiyo, walieleza mafanikio ya
kiuchumi yaliopatikana hapa Zanzibar na kusisitiza haja ya kuendelezwa ili
mafanikio zaidi yaendelee kupatikana.
Sambamba na hayo, viongozi
hao walieleza kuwa siri kubwa ya mafanikio hayo ni kuwepo kwa mashirikiano
pamoja na amani na utulivu hapa Zanzibar na kusisitiza kuwa hawatokuwa tayari
kuwaona watu wachache wakitaka kuivuruga amani iliyopo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment