Mhandisi Khamis
Massoud akitoa maelezo ya kiufindi katika barabara ya Mangwena kuelekea Gando
ambayo iliharibiwa na mvua za masika mwaka jana mbele ya Mshauri wa Rais Pemba
Mauwa Abeid Daftari alipofanya ziara ya kuitembembelea barabara hiyo
Hili ni eneo la
barabara ya Mangwena ambalo hapo mwaka jana liliharibiwa na mvua za
masika
Hili ni eneo la
barabara ya Mangwena ambalo hapo mwaka jana liliharibiwa na mvua za
masika
Mshauri wa Rais Pemba
Mauwa Abeid Daftari akieleza jambo mbele ya uongozi wa Wizara ya Mawasiliano na
Uchukuzi Pemba wakati alipofanya ziara ya kutembelea barabara huko Mgelema
(PICHA NA SAID ABDULRAHMAN PEMBA
Na Said Abdulrahman
Pemba
Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na usafirishaji Pemba imeombwa
kuzifanyia matengenezo ya haraka bara bara zote ambazo kwa sasa haziko vizuri.
Akizungumza
baada ya ziara yake aliyoifanya ya kutembelea baadhi ya barabara za Kusini na
Kaskazini Pemba,Mshauri wa Rais Mauwa Abeid Daftari, alisema ni vyema Wizara
hiyo kuchukua hatua za makusudi ili kuzifanyia matengenezo ya haraka ili ziweze
kupitika njia hizo katika kipindi hichi cha mvua zinazokuja.
Alifahamisha
kwa upande wa barabara ya Kipapo -Mgelema alisema hali siyo mbaya sana ila kuna
baadhi ya maeneo yanatakiwa kufanyiwa matengenezo madogo madogo ili wananchi wa maeneo hayo waweze kusafiri bila
ya usumbufu wowote.
“Madhumuni
ya kutembelea maeneo haya ni kutokana na sasa tunakabiliwa na mvua mkubwa,hivyo basi
ziara hii itatupa muamko ni sehemu gani ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi kwa
haraka ili mvua zitakapokuja wananchi wetu wasipate shida ya usafiri,”alisema
Mshauri huyo.
Mauwa
, alieleza kuwa nia ya Serikali ni kuitengeneza barabara hiyo ya Mgelema kwa
kiwango cha lami ,ila kwa sasa Wizara hiyo inamalizia kazi za maeneo mengine
ambayo tayari wameshaanza.
Akizungumzia
barabara ya Mangwena ambayo iliharibiwa na mvua za mwaka jana, Mshauri huyo
alisema kwa sasa barabara hiyo ni hatari na hivyo aliwaomba wenye vyombo vya
moto kupita katika njia iliyotengenezwa kwa muda ili kuwapa nafasi wajenzi
kuishughulikia.
“Kwa
sasa tuwaombe wananchi wetu kuacha kutumia barabara hiyo hasa wale wenye
vipando vikubwa ili kuwapa nafasi wenzetu wa Mawasiliano kufanya kazi zao kwa
urahisi,”alifamisha Mshauri huyo.
Sambamba
na hayo Mshauri huyo ,aliiomba Wizara hiyo kutengeneza mitaro ya maji na kuiweka
usafi katika hali ya usafi. ili wakati wa mvua maji yaweze kwenda sehemu
inayohusika.
Kwa
upande wa barabara ya Chake Chake – Wete kongwe,alisema tayari
imo mbioni kutengenezwa kwani mambo yote yameshakaa sawa na kuwataka wananchi
kuwa na moyo wa subra.
Kwa
upande wake , Ofisa Mdhamini wa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi Pemba, Ahmed
Hamad Baucha alisema kuwa barabara ya Kipapo-Mgelema imo katika harakati za
kujengwa kwa kiwango cha lami ila kwa sasa wanalizia barabara ambazo tayari
wameshazianza kuzifanyia kazi.
Alifahamisha
kwa upande wa barabara ya Mangwena ambayo iliharibika mwaka jana kwa mvua za
masika,alieleza kuwa walikuwa wanasuburi majibu kutoka kwa wataalamu ambao
wamechukua udongo wa hapo na kwenda kulifanyia vipimo ili kujua tatizo lake.
Mshauri
huyo wa Rais Pemba alitembelea Barabara ya Kipapo-Mgelema,barabara ya Chake
Chake –Wete kongwe, barabara ya Mangwena, Kuungoni pamoja na kuangalia barabara
ya kuingilia Ikulu ndogo Micheweni.
No comments:
Post a Comment