Habari za Punde

Tanzania na Kenya zaadhimisha mafanikio ya mahusiano ya kibiashara na kujadili mikakati ya baadae

Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Pindi Chana akitoa neno la ufunguzi katika Kongamano la biashara kati ya Tanzania na Kenya lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa cha Kenyatta Jijini Nairobi, Kenya tarehe 27 Aprili 2018. 
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Chris Kiptoo ambaye pia ni mgeni rasmi katika kongamano hilo la biashara akitoa hotuba ya ufunguzi wa ambapo alieleza kuna umuhimu mkubwa wa kuongeza mzunguko wa biashara baina ya Tanzania na Kenya pia ni wakati mwafaka wa kutumia fursa za rasilimali zilizopo baina ya mataifa hayo. 
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akihutubia katika ufunguzi wa kongamano la biashara ambapo alieleza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo tayari kufanya biashara na Jamhuri ya Kenya na kwamba maadhimisho ya kipekee ya wiki ya Tanzania nchini Kenya ni mwanzo wa kuimarisha na kuboresha ushirikiano uliopo na hivyo akasisitiza ni vema uma wa mataifa haya mawili ukajielekeza katika kununua na kuuza bidhaa baina yao. 
Kaimu Mkurugenzi wa Sera na uhamasishaji na mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF), Bi Neema Temba akitoa neno la utangulizi katika kongamano la biashara ambapo alisitiza umuhimu wa wafanyabiashara kuwa na ushindani unaojenga baina yao na pia alieleza sekta binafsi ni vizuri ikatambua na kuunga mkongo jitihada za serikali katika kuweka mazingira wezeshi ya biashara. 
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta binafsi, Bw. Nick Nesbitt akitoa taarifa ya utangulizi ambapo alieleza kuwa kongamano hilo ni fursa muhimu kwa wafanyabiashara kukutana na kujadili masuala mbalimbali ya biashara na uwekezaji na hivyo akaipongeza serikali ya Tanzania kwa jitihada walizozianzisha. 
Viongozi kutoka serikali ya Tanzania na Kenya wakifuatilia kongamano 
Wajumbe wakifuatilia Kongamano. 
Sehemu nyingine ya wafanyabiashara na wajumbe kutoka serikalini wakifuatilia kongamano. 
Wafanyabiashara wakifuatilia kongamano. 

Sehemu nyingine ya wafanyabiashara wakifuatilia kongamano.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.