Habari za Punde

Zanzibar Yapangwa kundi la kifo pamoja na ndugu zao Tanzania Bara Cecafa ya Vijana nchini Burundi

Kocha Mkuu wa Karume Boys Mzee Ali pamoja na wasaidizi wake akitoa mikakati ya mafunzo kwa wachezaji wa Karume Boys (hawapo pichani)

Na Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.

Timu ya Taifa ya Zanzibar ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 (Karume Boys) imepangwa katika kundi la kifo kwenye mashindano ya kombe la Chalenji yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi nchini Burundi April 14 hadi 28, 2018.

Habari zilizopatikana na Mtandao huu kutoka kwa CECAFA zinaeleza kuwa Zanzibar imepangwa kundi ‘B’ pamoja na ndugu zao Tanzania bara, Sudan na Uganda.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na baraza hilo inaonesha kuwa Zanzibar itaanza kampeni za kutwaa taji hilo, kwa kucheza na Sudan April 15 katika uwanja wa Gitega majira ya saa 7:30 za mchana.

Tayari Zanzibar imechagua wachezaji 20 na ipo katika maandalizi makali chini ya kocha mkuu Mzee Ali Abdallah, ambapo Vijana hao wapo kambi katika Hoteli ya Zanzibar Paradise International iliyopo Uwanja wa Amaan.

Katika Mashindano hayo yamepangwa makundi mawili yani A ambalo lenye timu za Kenya, Ethiopia, Somalia na wenyeji Burundi.


Michuano hiyo inatarajiwa kuanza April 14 katika viwanja vitatu tofauti nchini Burundi vikiwemo uwanja wa Ngozi, Muyinga na Gitega.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.