Habari za Punde

Agizia kikapu chako cha Ramadhaan kusaidia ndugu zetu Zanzibar, Tanzania

Agizia kikapu chako cha Ramadhaan kusaidia ndugu zetu Zanzibar, Tanzania
Assalaamu Alaykum WarahmatuLlaahi Wabarakaatuh

Mwezi mtukufu wa Ramadhaan umekaribia.

Jumuiya ya Al Iman ya Northamptonshire nchini Uingereza ni Jumuiya ya Waislamu wanaozungumza kiswahili imeamua kuendeleza “Kikapu cha Ramadhaan” (Ramadhaan Basket) kama tulivyoweza kufanikisha mwaka jana Bi idhni Llaah

Kwa Pauni  £15.00 tu unaweza kujipatia kikapu chako na mchango wako kama ni sadaka yako kwa ndugu zetu katika mwezi mtukufu wa Ramadhaan.

Tunakuomba kwa moyo mkunjufu, andaa kikapu chako sasa na Allaah ‘Azza wa Jall atakulipa kwa mchango wako kwa kuchangia Pauni 15.00 tu kwa kikapu kimoja. (unaweza kuongeza vikapu zaidi ukihitajia) 

Kwa mwaka huu kikapu chetu kitakuwa na:
Mchele  10kg
Unga ngano  5kg
Sukari    2kg
Maharagwe  2kg
Unga wa sembe 2kg
Mafuta ya kupikia 2lt.

Kikapu hichi kitakugharimu Pauni  15 tu kukinunua na kukigawa.

Kutuma mchango wako online Transfer, Lloyds Bank,  Sort Code 309609  Account 03539228
Tumia reference: ‘Ramadhaan Basket’

Kama utachangia kwa njia ya cheki hakikisha cheki imeandikwa na kulipwa kwa  Al – Iman Society of Northamptonshire
Na upande wa nyuma iandikwe:  ‘Ramadhaan basket’

Au unaweza kutuletea kwenye Msikiti wetu: Northampton Mosque & Islamic Centre, Clare Street, Northampton NN1 3JF 

Kwa maelezo Zaidi na ufafanuzi wasiliana na Amiyr wa Jumuiya: Ustaadh Abdulrazak +44 7951816208 au email iman@al-iman.co.uk

Al Iman Society of Northamptonshire ni Jumuiya iliyosajiliwa kama Jumuiya ya khiari yenye makaazi yake Northampton UK ikiwa na namba ya usajili  1117020 

Baaraka Llaahu fiykum

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.