Habari za Punde

Kampuni ya Kichina ya China Civil Yakabidhi Msada wa Vyakula Kwa Wananchi Waliopata Maadha ya Mvua za Masika Zanzibar.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud Mohammed akizungumza na Ujumbe wa Kampuni ya China Cilil Engineering Construction Corporation, walip inayoteIIVIL  ofika Ofisini kwake kwa kukabidhi Vyakula kwa ajili ya kuwasaidia Wananchi waliopata maafa ya Mvua katika sehemu mbalimbali za Unguja, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ofisi yake Vuga Zanzibar
MWAKILISHI wa Kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation David Yan, akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi msaada kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud, walipofika kukabidhi msaada huo wa Vyakula, hafla hiyo imefanyika katika Ofisi ya Makamu Vuga Zanzibar

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud Mohammed, akipokea mafuta ya kula kutoka kwa Mwakilishi wa Kampuni ya Ujenzi ya China Civil Engineering Construction Corporation, inayotengeneza barabara ya Bububu hadi Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja, kwa ajili ya Wananchi waliopata maafa ya mvua za masika Unguja, walikabidhi vyakula Mchele, Sukari na Unga wa ngano.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud Mohammed akitowa shukrani kwa msaada huo wa vyakula baada ya kukabidhiwa. na Mwakilishi wa Kampuni ya Ujenzi wa Barabara ya China CIVIL Mr. David Yan,hafla hiyo imefanyika katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Vuga Zanzibar.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.