Aidha, Dk. Shein Dk.
Shein ambaye pia, ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliwataka
Mabalozi hao kutowaunga mkono wale wote wanaofanya mambo kinyume na maadili ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kujitangazia kugombea nafasi za uongozi kabla ya
wakati uliowekwa ndani ya chama hicho.
Aidha, Makamo Mwenyekiti
huyo wa CCM Zanzibar alieleza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzbar katika
suala zima la ajira kwa vijana licha ya kuwepo kwa vijana wengi wanaomaliza
elimu ya juu na kuhitaji ajira ambapo inakisiwa karibu vijana 42,000 wamemaliza
kutoka vyuo vikuu vitatu vya Zanzibar wamemaliza masomo ndani ya miaka saba ya
uongozi wake.
Sambamba na hayo, Rais
Dk. Shein alitoa agizo kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji, na Nishati
kulitafutia ufumbuzi wa haraka tatizo la maji katika kijiji cha Kajengwa
Makunduchi.
Nao Mabalozi wa Wilaya
ya Kusini Unguja walitoa pongezi kwa Dk. Shein kwa jinsi anavyotekeleza vyema
Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kutumia
fursa hiyo kumpongeza kwa hotuba yake ya Mei Mosi mwaka huu aliyoitoa huko Mkoa
wa Kaskazini Pemba.
Pia walimpongeza kwa
nyongeza ya mishahara aliyoitoa mara nne ndani ya kipindi cha miaka saba ya
uongozi wake na kueleza kuwa hakuna nchi yoyote duniani iliyoweza kufanya hivyo
hatua ambayo inatokana na usimamizi mzuri wa mapato ya serikali anayoiongoza.
Mbali ya mafanikio
yaliyopatikana katika Wilaya hiyo, Mabalozi hao pia, walieleza changamoto
zinazowakabili ikiwa ni pamoja na migogoro ya ardhi, uvamizi wa maeneo ya
kilimo na misitu huku wakiiomba Idara ya Ardhi kutoa taaluma kwa wananchi
katika suala zima la uhakiki wa ardhi unaoendelea hivi sasa.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment