RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea
kuwachukulia hatua kali wawekezaji au waajiri wote wanaokwenda kinyume na
sheria za Serikali.
Amesema kuwa Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini sana mashirikiano ya Sekta binafsi na
kusisitiza kuwa wawekezaji au waajiri wanaodharau sheria au maslahi ya wananchi
hawatovumiliwa hata kidogo.
Dk. Shein aliyasema
hayo leo katika ukumbi mdogo wa Baraza la Wawakilishi, Wete, Mkoa wa Kaskazini
Pemba katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi),
ambapo Zanzibar inaungana na nchi nyengine duniani katika maadhimisho hayo.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa inasikitisha kwamba kuna baadhi ya wawekezaji na waajiri ambao wafanyakazi kuzikwamisha juhudi za
Serikali ambapo walijaribu kuupinga uwamuzi uliotolewa na kutishia kuwafukuza
wafanyakazi na kuweka visingizio mbali mbali ili waendelee kulipa mishahara
wanayoitaka bila ya kuzingatia sheria za nchi.
Hata hivyo, Dk. Shein
alisema kuwa amefurahi kuona kwamba hivi sasa wananchi wengi wanaofanya kazi
katika sekta binafsi, wameanza kufaidika na kiwango cha mshahara
kilichotangazwa na kutoa wito kwa taasisi ambazo bado hazijatekeleza agizo hilo
zitetekeleze kwa haraka.
Aidha, Dk. Shein alisisitiza
haja ya kupima afya kwa wafanyakazi wote na kuwashajiisha kufanya mazoezi
kupitia vikundi mbali mbali vilivyoanishwa ili kuwakinga na maradhi huku
akisisitiza kuwa UKIMWI bado upo hivyo tahadhari badozinahitajika.
Kutokana na wanawake
wengi hivi sasa kukumbwa na vifo vinavyotokana na ongezeko la maradhi ya
Saratani ya Shingo ya Kizazi, Dk. Shein aliwasisitiza wananchi kumuunga mkono
Mama Shein kwa kuzindua kampeni hiyo kwa upande wa Zanzibar na Makamo wa Rais
Mama Samia aliyezindua kwa upande wa Tanzania Bara mnamo tarehe 10 mwezi
uliopita.
Kadhalika, Dk. Shein aliwahimiza
wafanyakazi kuunga mkono juhudi za Serikali na jamii katika kupiga vita vitendo
vya udhalilishaji na unyanyasaji wa kijinsia jambo ambalo limekuwa ni tatizo kubwa nchini hasa katika miaka ya hivi
karibuni.
Rais Dk. Shein
alisisitiza kwamba vyama vya wafanyakazi lazima vitekeleze majukumu yao ya
msingi kwa kuzingatia haki na wajibu wa pande mbili na kueleza kuwa hatochoka
kuvihimiza vyama vya wafanyakazi, ili vizingatie kwamba haki na wajibu ni
watoto pacha.
Hivyo, Dk. Shein
alitoa pongezi kwa vyama mbali mbali vya wafanyakazi kupitia Shirikisho la
Vyama Huru vya Wafanyakazi kwa juhudi wanazozichukua katika kuyatetea na
kuyalinda maslahi ya wafanyakazi ambao ndio wanachama.
“Nakusisitizeni
viongozi wa vyama vya Wafanyakazi muendelee kushirikiana na Serikali katika
kuimarisha uwajibikaji, maadili pamoja na kuendeleza vita dhidi ya rushwa na
ubadhirifu wa mali ya umma”,alisema Dk. Shein.
Aidha, kuhusu tatizo
la ajira kama ilivyo katika mataifa mbalimbali duniani, Serikali inaendelea
kutekeleza mikakati yenye lengo la kuitafutia ufumbuzi changamoto hiyo ikiwa ni
pamoja na kutoa mikopo kwa vikundi mbali mbali vya wajasiriamali kupitia Mfuko
wa Uwezeshaji.
Alieleza kuwa Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuwaajiri vijana katika sekta mbali mbali
kwa kadri nafasi zinavyopatikana huku akieleza kuvutiwa na kauli mbiu ya
maadhimisho ya mwaka huu isemayo “Njia Pekee ya Kukuza Uzalishaji na Kuimarisha
Huduma, ni Kujadiliana na kujali Ushirikishwaji”, alisema Dk. Shein.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment