Na.Salmin Juma.- Pemba.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Jeshi la Polisi Kisiwani Pemba lafanikiwa kukamata dawa za kulevya katika zoezi linaloendelea, Kwa mujibu wa Taarifa ya Kamanda ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba RPC Shehan
Mohd Shehan.
Tokea tarehe 20
/ 05 /2018 Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Pemba lilianza kuendesha operesheni
maalum ya kupambana na uhalifu pamoja na madawa ya kulevya.
Miongoni mwa
matukio yaliyopatikana ni yafuatayo.
06/06 /2018 saa
9 jioni huko Minazini Chakechake, jeshi la polisi lilimkamata Husein Suleiman
Hassan (20) akiwa na unga unaodhaniwa kuwa ni madawa ya kulevya ambao alikua
ameufunga katika makaratasi ya gazeti, kwasasa mtuhumiwa yupo chini ya
uwangalizi wa jeshi hilo na hatua nyengine za kisheria zinafuata.
11/06/2018
mchana , hukohuko minazini chakechake , Jeshi lilimkamata Najim Ali Omar (54)
mkaazi wa misufini , alipatikana na pombe ya kienyeji aina ya gongo nyumbani
kwake,katika kidumu cha lita 10 ,mtuhumiwa yupo chini ya ulinzi na anaendelea
kuhojiwa ili kufikishwa mahakamani.
13/06/2018 saa
11:30 jioni huko Ole kianga,Yassir Nassor Hamadi (20) mkaazi wa Ole kianga
alikamatwa akiwa na majani makavu yanayosadikiwa kuwa ni bangi (nyongo 8) akiwa
ameyahifadhi ndani ya suruali,mtuhumiwa yupo chini ya uwangalizi wa jeshi la
polisi , hatua za kumuhoji zinaendelea.
15/06/2018, saa
2 usiku, chakechake mjini , Hassan Bakari Hassan (37) mkaazi wa misufini
chakechake amekamatwa akiwa na mirungi ndani Ya mfuko mwekundu, furushi moja
lililojaa, mtuhumiwa yupo chini ya jeshi la polisi kuhojiwa kisha kufikishwa
mahakamani.
16/06/2018 ,saa
9:30 jioni huko pujini dodo, Jeshi la polisi limemkamata Jizahibu Ali Amour
(24) akiwa na kete 51 zinazosadikiwa kuwa ni madawa ya kulevya , kete hizo
zilikua katika mfuko wa plastiki aliyokua ameubeba, jeshi la polisi limemkamata
na hatua za kisheria zinaendelea juu yake.
16/06/2018, 6:20
mchana
hukohuko pujini dodo,jeshi la polisi limemkamata Yahya Abdalla Omar (20)
akiwa na nyongo 11 zinazosadikiwa kuwa ni bangi .
17/06/2018, saa
3 asubuhi huko Mtambile jeshi la polisi lilimkamata Salah Mbarouk Salah (
43 ) mkaazi wa kichungwani chakechake
akiwa na kete 40 zinazodhaniwa kuwa ni madawa ya kulevya.
Wito
Jeshi la polisi
mkoa wa kusini Pemba linawataka wananchi hususan vijana , kuacha kabisa
kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya kwani sheria zipo macho na
zinamgusa kila atakaehusika.
Aidha Jeshi la
polisi linawataka wananchi kuishi kwa kufuata misingi mema ya kimaisha yenye
kuendana na sheria ili amani azidi kutawala kwa wote .
No comments:
Post a Comment