Habari za Punde

Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein Atoa Mkono wa Eid El Fitry Kwa Wazee wa Welezo na Nyumba ya Wazee Sebleni Zanzibar.

Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar Mhe. Maudline Casticio akisalimiana na Wazee wa Nyumba ya Wazee Sebleni alipofika kuwapa Mkono wa Eid El Fitry akimuwakilisha Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein.
Mkuu wa Wilaya ya Mjini Unguja Mhe. Marine Joe Thomas akisalimiana na Wazee wa Nyumba ya Wazee Sebleni alipofika kuwasalimiana na kumuwakilisha Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, kutowa Mkono wa Eid El Fitry katika makaazi yao Sebleni Unguja. 
Katibu Mkuu Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar Bi Fatma Gharib Bilal akizungumza na kumkaribisha Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar kutowa salamu za Eid El Fitry, kwa Niaba ya Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, alipofika katika makaazi yao Sebleni Unguja. 
Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar Mhe. Maudline Castico akizungumza na kutowa salamu za Mkono wa Eid El Fitry kwa niaba ya Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein.





No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.