Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Sheid Awasili Nchini Indonesia leo Kuaza Ziara Yake Nchini Humo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malaysia pia akiwakilisha Tanzania Nchini Indonesia Mhe.Dkt Ramadhani Kitwana Dau (kulia) mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Soekarno Hatta, Jakarta Indonesia leo, akifuatana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein pamoja na Viongozi mbali mbali,katika ziara ya kikazi ya siku saba kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mhe.Mohammed Jusuf Kalla,[Picha na Ikulu.]31/07/2018.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewasili nchini Indonesia leo kwa ajili ya ziara maalum ya kikazi kufuatia mwaliko wa Makamo wa Rais wa nchi hiyo Muhammad Jusuf Kalla.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Indonesia, Soekarno- Hatta, uliopo mjini Jakarta Dk. Shein alipokelewa na miongoni mwa viongozi wakuu wa Serikali wa Nchi pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malaysia ambaye pia anaiwakilisha nchi hiyo Ramadhan Dau.

Ziara hiyo ya Dk. Shein ambayo inatarajiwa  kuanza rasmi hapo kesho itaanza kwa  mazungumzo na mwenyeji wake Makamo wa Rais wa nchi hiyo Muhammad Jusuf Kalla na baadae kufanya mazungumzo na viongozi wengine mbali mbali wa ngazi za juu wa Serikali pamoja na viongozi wa sekta binafsi wa nchi hiyo.

Katika ziara hiyo, Rais Dk. Shein amefuatana na viongozi mbali mbali akiwemo Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko, Balozi Amina Salum Ali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa, Haji Ussi Gavu, na viongozi wengine wa Serikali.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein anatarajiwa kufanya ziara nchini humo ambayo atakutana na viongozi wakuu, kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo, kukutana na wafanyabiashara, kutembelea sehemu za utamaduni na zile za kitalii.

Dk. Shein anatarajiwa kurejea nchi Agosti 6, mwaka huu.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar.

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.