TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MAAMUZI YA SERIKALI YA
KUKISAIDIA KIWANDA CHA SUKARI CHA MAHONDA KUKILINDA NA KUJIENDESHA
KIBIASHARA
Ndugu
Waandishi wa Habari
Kwanza
naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana hapa tukiwa
wazima wa afya na tunaendelea vizuri na harakati za ujenzi wa taifa letu.
Kwa kipindi
kirefu Serikali ya Mapinduzi imechukua hatua za makusudi za kuinua uchumi wa
nchi katika sekta mbali mbali za kilimo, huduma na viwanda na hivi sasa
Serikali inajitahidi kuhakikisha uchumi wa Zanzibar unaimarika katika Sekta ya
Viwanda.
Kwa mantiki
ya kufikia lengo hilo Serikali imefanya jitihada kubwa ya Kukimarisha pamoja na
viwanda vyengine kiwanda cha Sukari cha mahonda kwa kukipatia wawekezaji ambao
watahakikisha wanakiimarisha, kukilinda na kuongeza uzalishaji.
Ndugu
Waandishi wa Habari
Serikali
imetafakari kwa kina haja ya kukilinda kiwanda hiki kwa madhumuni ya kulinda
ajira za moja kwa moja za vijana wetu na zile ajira ambazo wananchi wengi
watafaidika nazo kwa vile wataweza kuongeza uzalishaji wa miwa na kuwa na
uhakika wa kupata soko. Hii inatokana na uzalishaji wote wa miwa utakaozalishwa
ndani ya Zanzibar utauzwa katika kiwanda hicho.
Aidha,
kiwanda hiki kimejikita katika mapinduzi makubwa ya kilimo cha kijani kwa kuwashirikisha
vijana katika program zake mbali mbali. Kuongezeka kwa uzalishaji wa miwa
itapelekea kiwanda kuzalisha umeme ambao baadhi utatumika kwa uzalishaji
kiwandani na mwengine utatumika kwa wananchi.
Madhumuni
ya Serikali kuweza kufikia lengo la kukisaidia na kulinda ajira za vijana wake,
kwa hatua za muda mfupi Serikali itahakikisha Sukari yote ambayo inazalishwa na
kiwanda cha Mahonda inapata soko lake ndani ya Zanzibar, hali hii itapelekea
kiwanda kuendelea na uzalishaji na kuimarisha ajira na kipato kwa wananchi
wapatao 4000 wanaoshiriki katika uzalishaji wa miwa.
Ndugu Waandishi
wa Habari
Madhumuni
makubwa ya kuwaiteni hapa leo tarehe 3/7/2018 ni kuwafahamisheni dhamira hiyo
ya Serikali na kuwapa taarifa wafanya biashara wetu wakubwa (waagiziaji) wa
Sukari kuwa Serikali imeweka utaratibu maalumu wa kuwapatia waagiziaji maalumu
kibali cha uagiziaji wa Sukari kutoka nje kwa masharti kuwa watainunua sukari
yote inayozalishwa na kiwanda cha Mahonda.
Aidha,
Serikali imeamua utaratibu huo uanze mwaka huu wa fedha 2018/19 kuanzia tarehe
1 julai 2018. Kwa waagiziaji watatakiwa kuinunua sukari ya mahonda iliopo hivi
sasa ndani ya kipindi hiki cha mienzi miwili ili kukiwezesha Kiwanda kuendelea
na mipango yake ya uzalishaji. Napenda ifahamike pia uwongozi wa kiwanda cha
mahonda hautoruhusiwa kuuza sukari hiyo kwa watumiaji wa mwisho, hii itasaidia
kutengeneza mfumo mzuri wa uendeshaji wa biashara ya sukari.
Serikali
imeunda kamati ya kulisimamia jambo hili ndani ya Tume ya Ushindani halali ya
Kumlinda Mtumiaji wakishirikiana pomoja na waigizaji wa sukari na uwongozi wa
kiwanda cha mahonda.
Ndugu
Waandishi wa Habari
Nakuombeni
muifikishe taarifa hii kwa wananchi ili waifahamu vizuri na kuwaomba wananchi
kutokuwa na wasiwasi wa kupanda kwa bei ya sukari, kwani kilichofanyika hivi
sasa ni mfumo mzuri tu wa usimamizi na kutatua changamoto iliyojitokeza kwa
biashara hii ya sukari.
Ahsanteni sana kwa Kunisikiliza.
No comments:
Post a Comment