Serikali ya Mkoa wa Kusini Unguja imezibomoa nyumba kumi na sita katika eneo la Tunguu ambazo zimejengwa
kinyume na utaratibu katika eneo lililotengwa kwa ajili ya shughuli za
maendeleo za miradi ya serikali ikiwemo upanuzi wa majengo ya chuo kikuu cha Taifa Suza.
Akishuhudia tukio la kuvujwa
kwa nyumba hizo Mkuu wa mkoa wa Kusini Unguja mhe Hassan Khatib Hassan amesema
serikali mkoani humo imeamua kuchukua hatua hiyo ya kuzivunja nyumba hizo
kutokana na wananchi wa eneo hilo kushindwa kutii agizo lililotolewa miezi mitatu nyuma la kuvunja na
kuhama katika maeneo hayo ili kupisha serikali kuendelea na zoezi la usafishaji
wa eneo hilo kwa ajili ya matumizi yaliokusudiwa.
Nao baadhi ya wananchi ambao
wamebomolewa nyumba zao wanaoishi karibu na maeneo hayo wamelalamikia hatua
iliyochukuliwa na serikali ya kubomoa nyumba hizo walizokua wakiishi kwa muda
wa takriban miaka 45.
Wamesema hatua
iliyochukuliwa na serikali ya kubomolewa nyumba hizo imewapa wakati mgumu kwa
sasa kwani hawana sehemu nyengine ya kwenda kuishi na watoto wao na hawana
uwezo wa kumudu gharama ya ujenzi wa makaazi mapya kutokana na hali zao za
umasikini hivyo wameiomba serikali kuu kuangalia uwezakano wa kuwapatia fidia
ili waweze angalau kutafuta sehemu nyengine ya kujihifadhi na watoto wao.
Nae Kaimu Makamo Mkuu wa
chuo cha Suza dkt Haji Mwevura haji amesema ni vyema kwa wananchi kuhakikisha
kwamba wanafuata taratibu za uhaulishaji wa ardhi kabla ya kununua maeneo ili
kuepukana na matatizo yanayoweza kujitokeza.
No comments:
Post a Comment