Kikundi cha Ngoma ya Shomo Kizimkazi wakionesha onesho lao la kitambiko la Utamaduni wa Wananchi wa Mkunguzi wakati wa Sherehe za Siku ya Kizimkazi Day zilizofanyika katika viwanja vya Mkunguni Kizimkazi kuadhimisha Siku hiyo huadhimishwa kila mwaka mwezi wa Agusti kwa michezo mbalimbali ya kiasili na upikaji wa Vyakula vya Kiasili ya Zanzibar na Kizimkazi.
Mgeni rasmin Makamo wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alifuatilia onesho la ngoma ya shomo wakionesha jinsi utaalamu wa kufukua vitu vibaya, kushoto Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bara Zanzibar Mhe. Haroun Ali Suleiman na kulia Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hassan Khatib Hassan.
No comments:
Post a Comment