Habari za Punde

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Atembelea Maonesho ya Nane Nane Mkoani Morogoro Leo.

 
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akivishwa Skafu na Vijana Chipukizi wa Morogoro mara alipoingia kwenye Unjwa wa Maonyesho wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoani Morogoro.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kiondoni Bwana Hija Saleh akimpatia maelezo Balozi Seif alipotembelea Banda la Manispaa hiyo kwenye Maonyesho ya Nane Nane Morogoro.
Hiba ya Kitalu cha Manispaa ya Kinondoni kinavyoonekana kikiwa katika hali ya kupendeza ndani ya Uwanja wa Maonyesho ya Nane Nane Morogoro.
Balozi Seif  akiendelea na ziara yake ya kulikagua Banda la Maonyesho la Halmashauri ya Mkuranga liliomo ndani ya Uwanja wa Maonyesho wa Mwalimu Julius K. Nyerere Morogoro.
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akifurahia na kuridhika na vidhaa zinazotengenezwa na Mjasiri Amali wa Mkoa wa Tanga, Jina halikupatikana.
Balozi Seif akinunua moja ya bidhaa zilizotengenezwa na Kikundi cha Wajasiri Amali kutoka Mkoani Tanga kwenye Maonyesho ya Nane Nane Morogoro.
Moja ya Kitalu cha zao la tungule likionekana kupendeza kutokana na Utaalamu mkubwa uliotumika kwenye ukulima wake ndani ya Uwanja wa Maonyesho Mkoani Morogoro.
Moja ya Bwana la kufugia Samaki la Chuo Kikuu cha sokoni Mkoani Morogoro ambalo Balozi Seif na Ujumbe wake alipata muda wa kulitembelea.
 Balozi Seif akifurahia Ukulima wa Mpunga uliooteshwa katika mfumo wa Taaluma ya kisasa kwenye Kitalu cha Kanisa la Anglican Dayosisi ya Morogoro kiliomo ndani ya Maonyesho ya Nane Nane.
Balozi Seif  akiendelea na ziara yake ya kukagua mambo mbali mbali ndani ya Uwanja wa Maonyesho wa Nane Nane wa Mwalimu Julius K. Nyerere Mkoani Morogo.
Balozi Seif akimshangaa Panya aliyepewa mafunzo maalum kuchunguza na hatimae kugundua  miripuko ya Mabomu ndani ya Banda la Chuo Kikuu cha Sokoine Mkoani Morogoro.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na vyombo mbali mbali vya Habari mara baada ya kumaliza zaiara yake ya kutembelea mabanda mbali mbali ndani ya Uwanja wa Mwalim Julius K. Nyerere Mkoani Morogoro.
Picha na – OMPOR – ZNZ.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.