Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Nchi Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali ya Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Bibi Reem Ibrahim Alhashimy alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake uliofika nchini kufuatia ziara ya Rais.aliyoifanya mwanzoni mwa mwaka huu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Waziri wa Nchi Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali ya Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Bibi Reem Ibrahim Alhashimy (katikati) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake uliofika nchini kufuatia ziara ya Rais.aliyoifanya mwanzoni mwa mwaka huu.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na Waziri wa Nchi Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali ya Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Bibi Reem Ibrahim Alhashimy baada ya mazungumzo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake waliofika nchini kufuatia ziara ya Rais.aliyoifanya mwanzoni mwa mwaka katika Nchi hizo,[Picha na Ikulu.] 09/08/2018.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein ametoa pongezi kwa Serikali ya Nchi za Umoja
wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa kuleta ujumbe wa timu ya Wataalamu ikiwa ni
matokeo ya ziara yake aliyofanyika Januari mwaka huu katika umoja wa nchi hizo.
Dk. Shein aliyasema hayo
leo wakati alipokuwa na mazungumzo na Waziri wa Nchi, Ushirikiano wa
Kimataifa wa Serikali ya Umoja wa Nchi za Kiarabu (UAE) Reem Ibrahim Alhashimy
ambaye pia, anaongoza wataalamu kutoka nchi za umoja wa nchi hizo aliyefika
Ikulu mjini Zanzibar kwa ajili ya mazungumzo.
Katika maelezo yake Rais
Dk. Shein alieleza kuwa ujio huo umeonesha dhahiri kuwa viongozi wa kutoka
Serikali ya Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) wana hamu kubwa ya
kutekeleza makubaliano ya mazungumzo aliyoyafanya kati yake na viongozi hao.
Rais Dk. Shein alieleza
kuwa katika ziara yake aliyoifanya mnamo mwezi Januari mwaka huu katika nchi za
umoja huo ambako alikutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa umoja wa nchi hizo ambao waliahidi kuendelea kuiunga
mkono Zanzibar ameamini kuwa azma yao hiyo imeanza kutekelezwa kwa vitendo.
Aidha, Dk. Shein
alieleza kuwa azma hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kutekeleza miradi ya
maendeleo ambayo itatekelezwa kwa mashirikiano ya pande zote mbili.
Aliongeza kuwa wananchi
wa Zanzibar walipokea kwa furaha kubwa mazungumzo ya makubaliano yaliotokea
baina ya pande mbili hizo na hatimae uongozi wa nchi za (UAE) ulipowafiki
kuunga mkono mradi wa ukarabati wa hospitali ya Wete pamoja na ujenzi wa
barabara ya Chake Chake Mkoani.
Pia, Rais Dk. Shein
alieleza kuwa mbali ya miradi hiyo kwa upande wa kisiwa cha Pemba, miradi
mengine yote iliyobakia kwa upande wa kisiwa cha Unguja wananchi wote kwa
ujumla wamefurahia na kuonesha matumaini yao makubwa katika utekeleza wake
ambao utasaidia kujiletea maendeleo na kuimarisha uchumi wa nchi.
Pamoja na hayo, Rais Dk.
Shein alieleza namna miradi hiyo itakavyoimarisha uchumi wa Zanzibar sambamba
na kutekeleza vyema sekta za kiuchumi, kijamii na kimaendeleo ikiwemo sekta ya
utalii ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa Zanzibar.
Dk. Shein, pia, alieleza
kuwa umoja wa nchi za (UAE) una historia ya muda mrefu katika kushirikiana na
kuiunga mkono Zanzibar katika sekta mbali mbali za maendeleo ikiwemo sekta ya
afya ambapo hapo siku za nyuma ilisaidia hata katika ukarabati wa hospitali kuu
ya MnaziMmoja.
Sambamba na hayo, Dk.
Shein alieleza kuwa matokea ya ziara yake ambayo yalimkutanisha na viongozi
wakuu wa (UAE) akiwemo Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan Mrithi wa Mtawala wa
Abu Dhabi na Naibu Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi wa (UAE), Mtawala wa Ras-Al-Khaimah
Sheikh Saud Bin Saqr Al Qasimi, Sheikh Mohammed bin Rashid Al
Makhtoum Makamo wa Rais na Waziri Mkuu wa (UAE) na Mtawala wa Dubai pamoja na
Mtawala wa Sharjah Dk. Sheikh Sultan Mohammed Al Qasimi.
Nae kwa upande wake Waziri
wa Nchi Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali ya Nchi za UAE Reem Ibrahim
Alhashimy, alimueleza Rais Dk. Shein kuwa ujio wa Wataalamu hao kutoka (UAE) ni
ishara kuwa uhusiano na ushirikiano uliopo baina ya pande mbili hizo ni wa muda
mrefu hivyo ni vyema ukaimarishwa.
Alieleza kuwa viongozi
wan chi za umoja wa (UAE), umeazimia kutekeleza makubaliano yote yaliokubaliwa
kufuatia ziara ya Rais Dk. Shein katika nchi hizo.
Aliongeza kuwa wataalamu
wote waliokuwemo katika ujumbe huo anaoungoza watafanya kazi kwa kutembelea miradi
iliyokusudiwa kwa upande wa Unguja na wengine wataenda kisiwani Pemba hapo
kesho.
Waziri huyo alieleza
kuwa kutokana na miradi hiyo kuwa na umuhimu mkubwa katika maendeleo ya jamii
hasa katika masuala mazima ya miundombinu ikiwemo ya barabara, elimu, masuala
ya kijamii, afya na mengineyo itasaidia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Zanzibar
na wananchi wake.
Sambamba na hayo,
kiongozi huyo alipongeza mapokezi mazuri aliyoyapata yeye na ujumbe wake na
kuahidi kuwa (UAE) itaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuhakikisha yale
yote yaliokubaliwa katika matokeo ya ziara ya Dk. Shein katika nchi za Umoja
huo yanafanyiwa kazi kwa vitendo.
Miongoni mwa makubaliano
hayo ni pamoja na mradi wa ukarabati wa Hospitali ya Wete pamoja na ujenzi wa
Barabara ya Chake hadi Mkoani kisiwani Pemba.
Aidha, kwa upande wa
Unguja miradi itakayohusika ni mradi wa hospitali mpya ya Binguni, Mradi wa
ukarabati wa nyumba za Mji Mkongwe, Miradi miwili ya Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA) pamoja na Barabara ya Fumba-Uwanja wa ndege kuelekea mjini.
Katika timu hiyo ya
wataalamu 16 pia, umo ujumbe kutoka Mfuko wa ‘Khalifa Fund’ ambao shughuli zake
kubwa ni kuwasaidia wajasiriamali na wale wanaohitaji misaada ya aina mbali
mbali
Dk. Ali AbdulKareem Al
Obaidli ambaye ni Kiuu wa Kundi la masuala ya taaluma alitoa mwaliko kwa
Zanzibar kuhudhuria katika Mkutano mkubwa utakaofanyika mnamo mwezi wa Septemba
mwaka huu huko Abudhabi ambao utajikita zaidi katika masuala ya afya
utakaozikutanisha nchi mbali mbali duniani ambapo pia, wajumbe watapata fursa
ya kutembelea miradi mbali mbali ya afya nchini humo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment