Habari za Punde

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar Bi. Khadija Shamte Mzee, Amewataka Wahitimu wa Kidatu cha Sita Kufuata Maadili na Kujiheshimu Wakati Wate Wanapokuwa Katika Masomo Yao Ili Kutimiza Ndoto Zao.


Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar Bi. Khadija Shamte Mzee alizungumza na kutowa nasaha zake kwa Wanafunzi Wahitimu wa Kidatu cha Sita Zanzibar wakati wa kukabidhiwa zawadi zilizotolewa na Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ katika viwanja vya Watoto Kariakoo Zanzibar. ,
Naibu Mkurugenzi wa PBZ,Bi.Khadija Shamte Mzee aliahidi kwamba utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wanaofaulu vyema itakuwa endelevu kwani imedhamiria kujenga taifa lenye rasilimali watu wenye ujuzi  na utaalamu utakao saidia kuleta mabadiliko ya haraka kiuchumi.
Alisema ulimwengu wa sasa unahitaji wasomi na wataalamu wengi hivyo aliwashauri kujifunza elimu ya matumizi ya fedha na kujiandaa na bajeti hasa ikizingatiwa ndio msingi wa maisha ya mwanadamu katika kujipangia hatua za kimaisha.
Aliwahimiza kufuata maadili na kujiheshimu wakati wote wanapokuwa katika masomo kwani ni miongoni mwa mambo yatakayowasaidia kutimiza ndoto zao.
Katika sherehe hiyo wanafunzi waliopata daraja la 1.3 walikabidhiwa shilingi milioni 3,000.000 kila mmoja ambapo wanafunzi waliopata daraja la 1.5 walipatiwa shilingi milioni 1.5 na wengine wa daraja la 1.6 hadi 9 walipatiwa shilingi milioni 1,000,000.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.