Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, Amtumia Salamu za Pongezi Waziri Mkuu wa India.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya India Narendra Damodardas Modi, kwa kuadhimisha miaka 72 tokea Taifa hilo kupata huru wake.

Salamu hizo zilieleza kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana na ndugu zao wa Jamhuri ya India katika kusherehekea sikukuu hiyo adhimu ya uhuru wa Taifa hilo ambayo ambayo ni ya kihistoria.

Katika salamu hizo, Dk. Shein alimuhakikishia Waziri Mkuu huyo kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza uhusiano na ushirikiano wa kihistorin uliopo kati yake na India sambamba na kuvumbua maeneo mapya ya mashirikiano kwa maslahi ya pande zote mbili.

Dk. Shein alimtakia kiongozi huyo na familia yake pamoja na wananchi wote wa India afya njema na sherehe njema katika kuadhimisha siku hiyo ya adhimu kwa Taifa hilo na kumtakia mafanikio zaidi ya kiuchumi kwa madhumuni ya kulinufaisha Taifa hilo na wananchi wake kwa amani na utulivu mkubwa.

Jamhuri ya India inasherehekea siku ya uhuru wa Taifa hilo kila ifikapo Agosti 15 ya kila mwaka ambapo nchi hiyo ilipata uhuru wake kutoka kwa Wakoloni wa Kiengereza mnamo mwaka 1947 chini ya uongozi wa muasisi na Baba wa Taifa hilo Hayati Mahtma Gandhi.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.