YALIYOJIRI LEO AGOSTI 6, 2018 MKUTANO WA RAIS DK SHEIN NA WAANDISHI WA HABARI UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA ABEID AMANI KARUME
RAIS MHE DK SHEIN
# Ziara yangu ya Indonesia ilijielekeza katika sekta zifuatazo, Kilimo, Biashara na Kilimo, Uwekezaji, Ushirikiano baina ya Nchi mbili hizi, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar kwa ujumla.
# Sekta ya Kilimo tulizungumzia suala zima la maendeleo ya kilimo cha Minazi, kilimo cha Mwani na kuusarifu mwani na kuangalia kilimo cha Mpunga.
# Utalii tulizungumza juu ya utalii wenyewe na mwelekeo wake, elimu kuhusu Utalii na Kampuni inayowekeza kuhusu utalii. Tulizungumza na kupata uzoefu wao.
# tulitembelea Viwanda vya samaki tukapata uzoefu wao na kupata mwelekeo mzuri wa kazi zao.
# Tulizungum,za pia na Wafanya biashara wa Indonesia na kuwahamasisha kuja kuwekeza Zanzibar.
# Tulizungumza pia Kampuni ya Gesi nao wanahamu ya kuja kuwekeza Zanzibar katika Suala la kutafuta na kuchimba Gesi.
# Tulitembelea na kuona namna Mwani unavyosarifiwa na kuleta faida kwa Wakulima.
# Katika wiki mbili zinazokuja Wawekezaji katika kilimo cha Mwani watakuja na kufanya mazungumzo na ikibidi watusaidie kuweka hata kiwanda kidogo cha Kusarifu mwani ili kuleta tija kwa Wananchi.
# Wameahidi kutusaidia sana katika uwekezaji, Mafunzo ya watendaji wetu na kuongeza Idadi ya WAtalii watakokuja kuitembelea Zanzibar.
# Tulikubaliana namna ya kushirikiana na kupeana uzoefu baina ya Chuo chao cha Utalii na Chuo kikuu chetu cha SUZA.
# Tumekubaliana pia kupeleka Madaktari wetu katika Kituo kikuu kinachotumika kutibu maradhi ya Moyo ambapo tumekubaliana kupeleka Madaktari wetu huko wakapate uzoefu na wakwao pia waje kwetu kutufundisha.
# Siku za karibuni Ujumbe kutoka Indonesia utakuja hapa Zanzibar na kuja kufanya mazungumzo kupitia Bank yao ya Exim
# Kiujumla Watu wa Indonesia wakiwemo Viongozi na Wawekezaji wamefurahishwa na Zanzibar na wako tayari kuja Zanzibar hivyo ni jukumu letu kuwaalika ili kuleta mafanikio tunayotarajia.
# Watendaji wakuu niliofuatana nao nao pia watapata nafasi ya kuzungumza kwa undani kile ambacho tulikiona na kujifunza.
# Watu wako tayari kuisaidia Zanzibar hivyo ni vyema nasi kuweka mazingira mazuri ya kusaidiwa.
IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI (MAELEZO) ZANZIBAR
AGOSTI 6, 2018
No comments:
Post a Comment