Habari za Punde

Benitez na Pellegrini - Mameneja Nyota Waliojipata Wakivuta Mkia Katika Ligi

Manuel Pellegrini na Rafa Benitez.
Rafael Benitez and Manuel Pellegrini ni mameneja wawili ambao walikuwa wamezoea maisha ya hadhi ya juu, lakini ambao sasa wamejipata mkiani katika timu tatu za mwisho katika Ligi ya Premio wakiwa na Newcastle na West Ham baada ya mwanzo duni katika msimu.
Benitez alishinda Ligi ya Mabingwa akiwa na Liverpool mwaka 2005. pia amekusanya vikombe vya Ulaya akiwa na Valencia na Chelsea huku naye Pellegrini akishinda kombe la Premio na Manchester City.
Hivyo ni kwa njia gani mameneja hao wawili wenye ujuzi wa juu wanaweza kushughulikia matatizo yao na wanawezaje kuziongoza Newcastle na WestHam kuelea?
Newcastle bila shaka wamekuwa na wakati mgumu wakicheza mechi za nyumbani za Tottenham na Chelsea ni ile ya ugenini na Manchester City. Wakati mmoja wangeweza kupata ushindi ni wakati Kenedy alikosa penalti dakika za 96 huko Cardiff.
Tatizo la Benitez ni ukosefu wa mabao. Upande wa mhispania huyo umefunga mabao matatu tu kwenye mechi nne licha ya kutua kwake Salomon Randon kutoka West Brom.
Mkiani West Ham hawana pointi baada ya mechi nne.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.