Habari za Punde

Rais Dk Shein atuma salamu za pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China kwa kutimiza miaka 69



STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar                                                                                     27.09.2018    

---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Watu wa China  Xi Jinping kwa  kutimiza miaka 69 tokea kuundwa kwa Taifa hilo.

Dk. Shein, alieleza kuwa  kwa niaba yake binafsi pamoja na wananchi wote wa Zanzibar wanatoa pongezi kwa Rais Xi, wananchi wa China pamoja na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China kwa kutimiza umri huo wa Taifa hilo tokea kuasisiwa kwake.

Salamu hizo zilieleza kuwa Watu wa Zanzibar wanapata faraja na matumaini kutokana na maendeleo makubwa yanayoendelea kupatikana katika Taifa hilo la  China kwenye sekta mbali mbali za maendeleo na uchumi.

Aidha, salamu hizo zilieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na wananchi wake wataendelea kutoa ushirikiano sambamba na kuimarisha uhusiano mkubwa uliopo kati yao na ndugu zao wa China.

Pamoja na hayo, salamu hizo za pongezi zilimtakia afya njema na mafanikio ya muda mrefu Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jimping katika kuliongoza Taifa hilo.

Uhuru wa Taifa hilo ulitangazwa mnamo Oktoba 1, 1949.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.