Mkurugenzi wa Tehama Ofisi ya Rais TAMISEMI,Ndg. Erick Kitali akiwasilisha mada kuhusu Mifumo ya TEHAMA, katika mkutano mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) unaoendelea mkoani Dodoma.
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Mhe. Kiomoni Kibamba,akichangia Mada iliowasilishwa katika Mkutano wa 34 ya Taasisi hiyo uliofanyika Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Mkutano huo, wakiwa wanasikiliza kwa makini mada ya mifumo ilipokuwa inawasishwa wakati wa mkutano huo wa 34 wa Jumuiya hiyo.
(Picha zote na habari na Atley Kuni- OR TAMISEMI)
Na. Atley Kuni- OR TAMISEMI
Wajumbe wa Mkutano
Mkuu wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania Bara (ALAT), wamepata somo juu ya
mifumo inayo simamiwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR
TAMISEMI) na jinsi mifumo hiyo ilivyo saidia katika masuala mtambuka ya
kimaendeleo katika jamii.
Somo hilo limetolewa
na Mkurugenzi wa TEHAMA OR TAMISEMI, Ndugu Erick Kitali wakati wa Mkutano Mkuu
wa 34 wa Jumuiya hiyo unaoendelea mkoani Dodoma na kuwakutanisha wajumbe kutoka
Halmashauri 185 za Tanzania Bara.
Akitoa mada hiyo
Mkurugenzi huyo wa TEHAMA, alisema toka kuanza kwa mifumo mambo mengi yameimarika
ikiwepo suala la mapato ya halmshauri ambapo kupitia mfumo wa ukusanyaji wa
mapato ya ndani ya Halmashauri (Local Government Revenue Collection Information
System- LGRCIS), imewezesha halmashauri hizo kujiongezea mapato ya ndani
ikilinganishwa na hapo awali.
“Waheshimiwa wajumbe,
kupitia mifumo yetu hali ya makusanyo imeongezeka sana ikilinganishwa na
kipindi cha nyuma ambacho tulikuwa tunakusanya kwa risiti za kawaida” alisema
Kitali, na kutolea mfano katika maeneo
yetu ya kutolea huduma za afya hususan ni katika Hospitali za Wilaya ambapo makusanyo
yalikuwa kati ya Mil. 3 hadi 6 kwa mwezi, lakini pindi matumizi ya mifumo yalipoanza,
makusanyo yamepanda na kufikia Mil. 24 hadi 40 kwa mwezi.
Kwa upande wao
wajumbe hao wakichangia na kutoa ushauri walipongeza kazi nzuri inayofanywa na
wizara ya OR-TAMISEMI, huku wakitaka maboresho ya mtandao katika mifumo hiyo iweze
kuongeza ufanisi hasa katika maeneo ya pembezoni mwa nchi, ambapo mkonga wa
taifa bado haujafika.
Akichangia mada
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Wakili Kiomoni Kiburwa Kibamba, alisema katika
kuimarisha suala zima la Makusanyo Serikali iende mbele na kuwa na mawazo
mbadala juu ya (Point of Sell- POS).
“Mhe. Mwenyekiti
nadhani umefika wakati wa kuwa na mashine hizi za POS ambazo zitakuwa zinajazwa
Flot
ili kusaidia kuepusha hatari mbali mbali ikiwepo kukwepa wajanja wanao
chezea mashine lakini vile vile hali ya hatari yakupoteza mashine.” alisema
Kibamba.
Katika wasilisho hilo
lililopata wachangiaji wengi, Mkurugenzi Erick hakucha kuwashukuru wadau mbali
mbali ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa mawazo mbadala yakuboresha
mifumo.
“Kufanya kazi OR-TAMISEMI, haina maana ndio utakuwa
unaelewa kila kitu, huu ni mpangilio tu wa majukumu, sisi kama wataalam ndani
ya Wizara tunapokea mawazo yenye kujenga ili shabaha yetu yakuwahudumia
wananchi iweze kufikiwa hivyo tunapokea mawazo yenye tija na kuyafanyia kazi
kwa manufaa ya taifa” alisema Kitali.
Wasilisho hilo ambalo
liliwasilishwa katika mkutano huo wa 34, lilihusiaha mifumo ya Tovuti za Mikoa na Halmashauri (Government
Website Framework GWF), ambao upo kwenye Halmashauri 185 na mikoa 26 nchini,
mfumo wa Malipo unatumiwa na halmashauri (Epicor) na mfumo wa Mipango na bajeti (Planning Budgeting
and Reporting PlanRep).
Mifumo mingine iliyo
wasilishwa katika kikao hicho ni Mfumo wa taarifa za Shule (School Information
System SIS), mfumo wa Vibali vya kusafiria nje ya nchi (eVibali), Mfumo wa kukusanya,
kuchambua na kutoa taarifa ya takwimu ya Elimu Msingi (Basic Education
Management Information System BEMIS), Mfumo wa Uhasibu na Utoaji taarifa kwa
ngazi ya kituo (Financial Facilities Account and Reporting System FFARS) pamoja
na mfumo wa kukusanya, kuhifadhi na kutoa taarifa za kitabibu (Government of Tanzania Health Management
Information System GoTHoMIS).
Mkutano mkuu wa wa 34
wa Jumuiya ya Mamlaka za Mitaa ALAT,unafanyika mkoani Dodoma katika ukumbi wa Jakaya
Kikwete na umewashirikisha Wenyeviti,Mameya, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali
za Mitaa, watendaji kutoka OR-TAMISEMI pamoja na wadau mbali mbali wa maendeleo
waliopata mialiko ya mkutano huo.
No comments:
Post a Comment