Taifa Stars wameshinda magoli mawili yaliyofungwa na mshambuliaji wa Difaa El Jadida ya Morocco Saimon Msuva katika dakika ya 29 akipokea pasi ya Mshambuliaji wa GRC Genk Mbwana Samatta. Mpaka Mapumziko Taifa Stars wanatoka kifua mbele kwa goli 1-0.
Katika kipindi cha Pili, Samatta aliipatia Taifa Stars goli la pili akimalizia pasi ya Mudathiri Yahya, akifuta lawama baada ya kukosa penati katika kipindi cha kwanza.
Taifa Stars walifanya mabadiliko ya kumtoa Abdi Banda na kuingia John Bocco, Mudathir nafasi yake ikichukuliwa na Feisal Toto.
Katika kipindi cha Pili, Samatta aliipatia Taifa Stars goli la pili akimalizia pasi ya Mudathiri Yahya, akifuta lawama baada ya kukosa penati katika kipindi cha kwanza.
Taifa Stars walifanya mabadiliko ya kumtoa Abdi Banda na kuingia John Bocco, Mudathir nafasi yake ikichukuliwa na Feisal Toto.
No comments:
Post a Comment