Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein Akihutubia Mkutano wa Blue Economy Nchini Kenya leo.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi Endelevu wa Bahari, (Sustainable Blue Economy Conference ) katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta Jijini Nairobi, akimuwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli.

Na.Suzan Kunambi.Nairobi Kenya.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,amesema Tanzania imejidhatiti katika kutoa ushirikiano unaohitajka katika utungaji wa sera na sheria mbali mbali zinazohusu sekta ya  uchumi wa bahari pamoja na kushiriki katika kutafuta nyenzo na rasilimali muhimu katika utekelezaji wa mipango iliyopangwa  katika sekta hiyo.

Dk. Shein aliyasema hayo leo katika ufunguaji  mkutano wa uchumi endelevu wa bahari kwenye ukumbi  wa Kenyatta Mjini Nairobi,wakati akitoa tamko la Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu mipango ya hivi sasa na baadae  katika kuendeleza nyanja uchumi wa bahari.

Alisema kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inategemea sana rasilimali bahari, mito na maziwa katika shughuli muhimu za kiuchumi na kijamii . Alieleza kwamba rasilimali hizo  zinaiunganisha  Jamhuri ya Mungano wa Tanzania  na mataifa mengine duniani katika sekta ya usafiri na mawasiliano, sambamba na kutumika katika  kuimarisha biashara,   utafutaji wa madini,  uendelezaji wa sekta ya nishati, kukuza uvuvi, utalii   na shughuli nyengine za kiuchumi na kijamii.

Alifahamisha kwamba kutokana na umuhimu wa rasilimali  hizo katika kuleta mageuzi ya kiuchumi na utekelezaji wa mikakati ya kupunguza umasikini, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa  mstari wa mbele katika  kupanga na kutekeleza mipango yenye lengo la kuziimarisha  na kuzilinda rasilimali hizo  dhidi ya changamoto na   athari mbali mbali; zikiwemo zinazosababishwa na shughuli za binaadamu.

Dk.Shein  alizibainisha  baadhi ya  athari na changamoto  hizo, ikiwa  ni pamoja na  uharibifu wa mazingira, ukame, kuongezeka kwa kina cha maji ya bahiri na majanga mbali mbali yanayaosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.
Alihimiza  haja ya  mataifa duniani pamoja na taasisi za kitaifa na kimataifa kuungana pamoja kwa ajili kupanga na kutekeleza mikakati madhubuti zaidi  itakayowezesha kuondoa changamoto hizo. Alieleza kwamba juhudi za pamoja zinahitajika hivi sasa, katika utekelezaji wa  mipango na ajenda za kuimarisha uchumi wa bahari katika ngazi za kitaifa na kimatafifa  kwa kuzingatia mipango iliyopo hivi  sasa na inayoendelea kupangwa.

Vile vile, asisitiza kwamba ili kupata mafanikio ya kweli katika katika kupanga na kuteleza mipango ya uchumi wa bahari na lazima sekta binafsi na jamii kwa jumla zishirikishwe kikamilifu.

Alimalizia kutoa tamko hili kwa  kuelezea imani yake kwamba maazimio yatakayopitishwa  katika mkutano huo, yakakuwa na mchango  mkubwa katika  kuendeleza uchumi wa bahari na kutoa mwelekeo mpya katika kuyafikia malengo Endelevu ya dunia  na kuimarisha ustawi wa  watu wote duniani.

Aidha Dk. Shein alitoa  shukurani na pongezi  kwa Serikali ya Jamhuri  ya Kenya  pamoja na Serikali ya Canada na Japan kwa  kuandaa mkutano   huu maalum wa Uchumi Endelevu wa Bahari.

Mapema akifungua mkutano huo Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya aliwashukuru wajumbe kutoka pande mbali mbali za Dunia kwa kushiriki kwa wingi katika mkutano huo uliolenga kuweka mikakakati itakayosaidia kutumia bahari,mito na maziwa kwa kukuza uchumi wa nchi na rasilimali hizo.
Akitoa tamko la Serikali yake Rais Kenyatta alielezea dhamira na muelekeo wa 

Serikali hiyo katika kuendeleza na kuzisimamia uchumi wa bahari na kusema kuwa Kenya itashirikiana na nchi mbali mbali na jumuiya za kimataifa katika kuendeleza uchumi huo wa bahari.

Mkutano huo wa siku tatu  uliondaliwa na Serikali ya Kenya kwa kushirikiana na Canada na Japan umeshirikisha nchi 180 na washiriki zaidi ya 13,000 kutoka taasisi mbali za binapsi,za kiserikali,wajasiriamali na makundi ya vijana na wanawake na watu wenye ulemavu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.