- Hupatikana kwa wingi Mkoa wa Mjini Magharibi
- Singo na Masaji hufanywa na wanawake
- Serikali yaonekana bado imelifumbia macho
Na
Mwandishi wetu , Zanzibar
Utamaduni
(culture) ni nyenzo muhimu katika maisha
ya mwanaadamu na hata taifa kwa ujumla, kwani ndio unaompangia vipi aishi.
Wataalamu
tokea zama na tangu waliwahi kutuambia kuwa asilimia 99 ya wakaazi wa Zanzibar
ni waislamu, hivyo bila ya shaka tokea zama hizo waliishi katika misingi ya
dini hiyo pamoja na zile mila za kizanzibari walizokubaliana.
Nikitaja
asilimia hiyo kwa wazanzibari
isifahamike vibaya kuwa hakuna waumini wa dini nyengine, wapo na ni wazaliwa
haswa wa visiwa hivi.
Makala hii
hailengi kuelezea udini, bali inakusudia kueleza umuhimu wa utamaduni pamoja na
athari zake hasa pale watu wanapoanza kuweka pembeni utamaduni wao na kufuata
kwengine kunapowadanganya kuwa kunawafaa.
Katika
kuutunza utamaduni wa Mzanzibari , serikali imekua ikifanya jitihada kubwa
kuhakikisha utamaduni haupotei wala kubadilika lengo ni kuonesha kuwa utamaduni
ni nyenzo muhimu katika maisha.
Dhana ya Utamaduni
ni dhana pana, ni mfumo mzima wa maisha ambao wananchi wanaishi kupitia mila , silka
na desturi hizo, miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na ndoa ambapo ndani yake kunapatikana kitu kiitwacho “SINGO”.
Nimegusia
ndoa kwakua katika mila na tamaduni za kizanzibari ili ufanye tendo la JIMAI ni lazima utangaze ndoa,
ukamilishe masharti yote
ukabidhiwe mke na ndipo unapokua
huru kwa tendo hilo, kinyume chake hata uwe na watoto 100 na wake unaowajua
wewe ikiwa umewapata nje ya ndoa hilo ni kosa tena la kisheria kwa wazanzibari, maana utamaduni wa Mzanzibari
unakwenda sambamba maadili ya Uisilamu.
Ingawa
serikali inajidhatiti katika jitihada za kuhifadhi utamaduni huo lakini bado
kuna baadhi ya taasisi zinarejesha nyuma juhudi hizo na kwa mwendo kasi zinavuruga
tamaduni tofauti na athari zake
zimeshaanza kujitokeza .
Taasisi hizo
zipo nyingi lakini leo nitazungumzia moja tu kati ya hizo kutokana na
uchunguzi niliyoanza kuufanya masiku
kadhaa yaliyo nyuma.
Nchini
Zanzibar kumejitokeza Saluni za kiume
ndani yake kuna wafanyakazi wakike wanaoshughulika na ufanyaji wa singo (scrub)
pamoja na masaji (kukanda mwili) na wanaofanyiwa ni wateja wakiume wanaofika
kupata huduma.
Saluni hizi zinapatikana kwa wingi ndani ya Mkoa wa Mjini
Maghribi Unguja, mkoa mama katika nchi
hii ingawa kule Pemba pia zimeshaanza kuingia.
Inasemekana
kuwa saluni hizi kwa kiwango kikubwa zinaharibu utamaduni wa mzanzibari, ni
kwasababu, kwanza ni kinyume na tamaduni , mila na silka za mzanzibari, mwanaume kusingwa na kukandwa kimahaba
anastahili kufanyiwa na mkewe tu, na mwanamke afanyiwe na mumewe, iweje leo
tamaduni hizi zikanyagwe na kufinyangwa kisha watu wabakie kimya !
Mengi yaliyojificha katika saluni hizi nitakujuulisha ili kujua kunanini ndani yake,
au ile dhana iliyonifanya kufuatilia jambo hili si ya kweli, nikaamua kulivalia
njuga na mengi niliyagundua.
Nilikwenda
katika saluni moja kwa mchina Mombasa njia ya kuelekea Mpendae, kulikua na wanawake
wasiopungua watatu (3) mmoja kati yao nilimuuliza.
Sista mambo
vipi?
Poa tu mzima
?
Mzima sijui
wewe?
Nami mzima
Ok poa, kuna
huduma ya kufanya scrub (singo ) hapa ?
Ndio ipo,
karibu ndani.
Alinichukua
moja kwa moja hadi katika chumba chake maalum, ndani ya chumba hicho tulikua
watu wawili tu (mimi na yeye).
Nimetangulia
kusema ni chumba chake kwa sababu kulikua na vyumba tofauti na kila mfanyakazi
inaonekana anachumba chake kwa mujibu wa mazingira yalivyokua.
Akanitaka
kuketi katika kiti, baadae akanishika kichwa na kunilaza taratibu, kisha
alinifungua vifungo vya fulana, baadae akaja na maji ya uvuguvugu na kitambaa
na kuanza kunipangusa.
Mikono yake
ilifika hadi chini ya shingo na kunipapasa kifua kwa hanjifu nyepesi na laini,
hayo ni maandalizi tu ya kufanyiwa singo .
“Geuka
kidogo tazama juu” aliniambia mwanamke huyo, sikua mkaidi.
Alianza
kunipaka (mafuta ya kusugulia) na kuanza kunisinga, “unajisikiaje na huu unaotoka ni uchafu utatakata vizuri tu,”aliniambia
mrembo huyo.
Ilikua ni
mazingira magumu sana kwangu lakini kwakua nimeamua kuchunguza ukweli juu ya
utamaduni unavyoharibiwa nilijikaza kiume kwakua wananchi wanataka kuufahamu
ukweli katika mambo yaliyojificha.
Niliamua
kupenyeza maneno matamu ili kuhakikisha mbali na hili kuna lipi jengine?
“yaani leo
najisikia raha sana kama nipo peponi, mtoto utaniuwa mie” akajibu “haha…
kawaida tu mbona”
“samahani
naweza kupata kampani yako leo usiku alau nijisikie mwenye bahati, maana nataka
kukufaidi mtoto” alijibu “wewe tu mimi mbona sina tatizo”.
Alinisinga
vizuri baadae akanikosha tena kwa maji ya uvuguvugu kisha akaniingiza chumbani
kumaliza tuliyoyazungumza.
“Niambie
sasa , kwani wewe unataka vipi” aliniuliza binti huyo
Nikamjibu
“kama nitakupata usiku wote wa leo itakua vizuri mana inaonekana upo vizuri
sana katika mambo yetu” akajibu “ok sawa kwangu hakunashida, utanilipa shilingi
70,000 na kama kukupunguzia tufanye shilingi 60,000 tu”
Tulikubaliana
hivyo, na hapo nikagundua , mbali na
singo zinazofanyika lakini kuna uwezekano mkubwa wa kufanyika biashara ya ngono
(ukahaba)
Nasema hivi
kwa sabau, kama utakumbana na huduma hii na jinsi walivyo wajuzi katika kazi ni
lazima tu utamsifia hapo hapo au ndio utaomba kwenda kumalizana kwa jinsi anavyofanya
ujuzi wake katika kazi ( kwa sauti na vitendo)
Kwa lengo lilelile
la kujiridhisha nilikwenda katika saluni nyengine (njia ya kuelekea Amani Mwanakwerekwe
mkabala na car wash) nako pia nilihitaji huduma ya singo ambayo ni shilingi
3,000 karibu ya saluni zote.
Na
nikaongeza huduma , sasa nikahitaji na masaji (kukandwa mwili) hii ni shilingi
30,000
Alikuja
mwanamke mzuri aliyetimia, kama kawaida aliniweka katika kiti na kuanza
kunipangusa, huyu alimzidi wa awali, alikichukua kichwa changu na kukiweka
chini ya kifua chake na juu ya tumbo (katikati) huku akinipangusa.
Hali ilikua
ngumu sana pia nilivumilia hadi akamaliza kazi yake, baadae aliniita chumbani
kama kawaida kwa lengo la kunifanyia masaji.
“vua nguo
nianze kukufanyia” alisema mwanamke huyo, aliashiria niwe mtupu zaidi ya pensi
au nguo ya ndani kama ninayo.
Ukweli
nilishindwa , nilijibabaisha kiume nionekane nimeghairi , ingawa hakuonyesha
kuridhika huku akinilaumu kwamba nimeshamkosesha pesa.
Pia nilitaka
kujiridhisha kwa mara nyengine tena juu ya biashara ambayo nina wasiwasi
huwenda ikawa inafanyika chinichini (ukahaba wa mtu mmoja mmoja).
Nilimuuliza
“hivi nikitaka nikuchukue ili ukanifanyie masaji kwangu itakuaje?” alijibu “
tatizo nipokazini , kama siku nakua frii hakunashida labda jaribu mwengine
unayemuona anakuvutia”
Alimaanisha
nijaribu mwengine humo humo katika wasichana wanaofanyakazi.
Kauli hii
inaashiria nini ? ni kwamba ukimuona anaekuridhi katika dada hao unaweza
kuzungumza nae na kuondokanae inategemea vipi munavyokubaliana, na sitaki
nizame kukuelezea biashara hii , mada yetu ni utamaduni wa singo na kukandana.
Hii ndio
hali kwa saluni karibu zote unazoziona kisiwani Unguja, maadili ya kizanzibari
yamekua yakipotea siku hadi siku, tangu lini mwanaume kufanyiwa singo na
asiyekua mkewe,
Bila ya
shaka kupitia matendo hayo kunazaliwa athari nyingi miongoni mwa hizo ni huko
kurahisika tendo la ngono kuwa ni kitu cha kawaida.
Kwa kuwa
wateja wengi wa huduma hizi ni vijana ingawa wamakamo na wazee wamo niliamua
kuchukua mawazo yao juu ya uwepo wa saluni hizi na nilikutana na kijana wa
miaka 25 hadi 27 (jina linahifadhiwa) alisema, saluni hizo zinaharibu utamaduni
wa nchini.
Kwani
kisheria kuna watu maalumu wanaopaswa kukusugua “pia hata biashara ya ukahaba inafanyika,
wakati anakufanyia scrub (singo)
hapohapo munapatana kisha mutajuana munakutana wapi” alisema kijana huyo.
Mwananchi
mwengine (dereva wa daladalaya K/samaki) alisema “kuna uwezekano mkubwa wa
kufanya ngono, siku moja nilikwenda kupata huduma, hee! mwanamke kaniinamishia
maziwa chini yangu huku ananitega , yaani ni mimi tu mwenyewe kutamka”alisema
mwananchi huyo.
Akielezea kwa hamasa aliniambia “maadili wanayaharibu
kwetu hakuna vitu hivi” mwisho wa kunukuu.
Nilipowauliza
ni kwanini wanakwenda katika saluni hizo, wengi walijibu kuwa, ni saluni za
kawaida na hakuna ubaya kuingia hasa kwa kunyoa nywele.
Sheikh
Khamis Bin Gharib kutoka Afisi ya Mufti Zanzibr nilipomgusia suala hili alisema,
dini imekuja kukataza mambo yote yanayoshawishi kufanya zinaaa pale ALLAH SW aliposema
katika qur an ‘’wala musiikaribie zinaa’’
“kila jambo linaloweza kumshawishi mtu kufanya zinaa jambo hilo ni haramu, ikiwamo mas ala ya
saluni ambayo mtu akienda anafanyiwa masaji na mwanamke ambae si halali yake,
yote ni haramu na nikuikaribisha zinaa”alisema Sheikh Khamis
Akiendelea
kufafanua zaidi alisema, kugusa kumekatazwa, kutazama kwa makusudi kumekatazwa ,alisema
jambo lolote linaloweza kuamsha hisia za mtu kufanya haramu jambo hilo
limekatazwa katika dini ya kiisilamu.
Kwa upande
wake Dk Omar Abdalla Adam Katibu Mtendaji, baraza la Sanaa na Utamaduni Zanzibar
alisema , Zanzibar ina mila, silka, na desturi zake pia watu wanaheshimiana.
“mwanamme na
mwanamke wanafanyia masaji ndani, hilo jambo halikubaliki na si sahihi wala si
katika utamaduni wa Zanzibar” alisema katibu huyo.
Alisema
masaluni hayo yapo na kuna baadhi ya vijana hawaridhiki lazima waende katika
saluni hizo, hivyo hao wenyewe ndio wanaosababisha kuwepo kwa matendo hayo.
Akizungumzia
msimamo wa serikali katika jambo hilo alisema serikali haikatazi uwepo wa saluni , lakini kama kuna matendo ambayo yapo
kinyume na utamaduni, hayo hayakubakili.
“wanaofanyiwa
hivyo si watoto , ni watu wazima, kila mmoja ajione kuwa yeye ni mzanzibari na
heshima zake, serikali itatoa taaluma kwa wananchi na kama kuna mtu anataka
kusingwa amwambie mkewe au kufuata utaratibu mwengine” alisema katibu huyo.
Mmoja kati ya
wahusika wa utoawaji wa Leseni za biashara za saluni kutoka Baraza la
Manispaa Mjini Zanzibar(jina limehifadhiwa) alisema “sipingi, kuna uwezekano mkubwa wa kufanyika biashara
ya ukahaba, huwa tunayaona, pia maadili yanavurugwa sana maana kivazi tu cha mwanamke kinasema mimi
nipo tayari kwa kila kitu” alisema afisa huyo
Alisema kawaida wanakua na utaratibu maalum wa
kuzikagua saluni na nyengine kuzifungia kabisa ikibainika kuwa hawajalipia kodi
lakini hawana utaratibu wa kutazama maadili ingawa mazingira yanaonyesha kuwa
tamaduni zinaharibiwa.
“ Masuala haya nilishayaripoti ingawa sio rasmi,
lakini kwa jinsi unavyonieleza nitayaripoti rasmi na kuyatilia mkazo ili
kuhakikisha maadili yanazingatiwa katika utoaji wa leseni kwa saluni hizi”
alisema
Mwisho kabisa alisema, endapo kutapitishwa utarabu wa
kuzungatia maadili katika utolewaji wa leseni hawatosita kuifungia saluni
yoyote pale itakapoonekana kukiuka sheria hiyo.
Uchunguzi
uliyofanywa na mwandishi wa makala hii umegundua kuwa, iwapo serikali
haitolivalia njuga kwa nguvu zote suala hili , utamaduni wa mzanzibari unaweza
kupotea haraka sana ikabaki kuwa kumbukumbu.
Kama kweli
tunathamini utamaduni wetu kila mmoja awe mchunga kwa mwenzake kuhusu jambo
hili, saluni hizi naziweka katika orodha ya majanga makubwa yanayoifika nchi
ndogo ya Zanzibar, tulipo toka sipo tunapokwenda, lazima tuwe macho tutamalizika.
ahsante sana muandishi wa makala hii, yaonyesha ni jinsi gani unajitambua na kuumwa na utamaduni wetu mzuri wa kizanzibari. Hongera sana.
ReplyDeletenataka kuchangia kidogo kwenye kauli hii ya Katibu mtendaji aliesema hivi:-
" Akizungumzia msimamo wa serikali katika jambo hilo alisema serikali haikatazi uwepo wa saluni , lakini kama kuna matendo ambayo yapo kinyume na utamaduni, hayo hayakubakili.
“wanaofanyiwa hivyo si watoto , ni watu wazima, kila mmoja ajione kuwa yeye ni mzanzibari na heshima zake, serikali itatoa taaluma kwa wananchi na kama kuna mtu anataka kusingwa amwambie mkewe au kufuata utaratibu mwengine” alisema katibu huyo."
sikubaliane naye kwani hii ni kufumbia macho tatizo, kwani nani asiejua kuwa kuna wenzetu wao wanakuja na biashara zao na wateja wao? kisha tena baada ya muda na vijana wetu wasiojitambua huanza kuvutiwa na kujiunga na biashara hizo. kwa mfano;
biashara ya pombe na bar, wamekuja nayo mwanzo wateja wakawa wao sasa vijana wetu wengi wanashiriki kikamillifu.
mfano wapili ni biashara ya bodaboda, wamekuja nayo na wateja mwanzo walikuwa wao tu sasa na sisi tushaingia kikamilifu.
mfano wa tatu biashara ya ukahaba, walikuja nayo mwanzo mwanzo wateja walikuwa wao, sasa na sisi tumo tele.
na mifano mengine tele ipo, kwa hivyo tunachotakiwa kufanya ni kuzuia vishawishi, tushaona hizi saluni zitatuharibu kwa nini tusubiri ushahidi wa mnyamwezi na kusema wanoenda ni watu wa wazima na akili zao? basi hao watoto nao watakwenda tena kwa wingi na wataiba pesa za wazee wao na za wazee wa wenzao na hapo ndio balaa litakapozidi, maana ngono nayo ni kilevi, akishazowea mtoto mchezo wa kuchezewa atataka kila wiki aende.
uungwana na usmart tusisubiri yaharibike tuzuie mwanzo, saluni huduma iwe moja tu ya kunyoa au kukata nywele za kichwani tu ikiwemo masharubu na ndevu, basi, yalobaki kila mtu akafanye kwake. kwanza watu wenyewe hata kodi hawalipi mtu anapewa huduma zote hizo analipa karibu laki 1 hakuna risiti wala nini, hapalipwi kodi, na utamaduni wetu unaharibiwa.