Raya Hamad
OR-KSUUUB
Wafanyakazi wa
sekta ya utumishi wa umma wametakiwa kujituma na kufanya kazi kwa uaminifu na
uadilifu katika kuitumikia nchi.
Waziri wa nchi
Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Haroun Ali
Suleiman ameeleza hayo kwenye sherehe ya
kuwaaga wastafu wa ofisi hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo
mazizini, unguja.
Mwalimu Haroun
amesema serikali ya Mapinduzi Zanzibar ya awamu ya saba imefanya mambo mengi
kwa maendeleo ya wananchi na mabadiliko
ya kwenye utumishi wa umma ikiwa ni pamoja na kuongezewa pencheni pale
mfanyakazi anapostaafu kwa lengo la
kuongeza ufanisi katika utumishi serikalini.
Aidha
amewapongeza wastafu hao kwa kuwa wazalendo na kuweza kufanya kazi kwa uadilifu kwa muda wote
walipokuwa watumishi wa serikali na kustaafu wakiwa nasifa nzuri na mfano wa
kuigwa.
Nae Naibu Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora ndugu Seif Shaaban Mwinyi amasema mnamo mwaka 2011Serikali ilifanya utafiti wenye lengo la kuimarisha mazingira ya wastaafu
kabla na baada ya kustaafu .
Ameyataja mazingira
hayo kuwa ni pamoja na kuongezewa pencheni, kuhakikisha wastaafu wanapatiwa
mafunzo kabla ya kustaafu, kupewa taarifa ya kustaafu miezi sita kabla, kupatiwa
cheti cha heshima, kuagana na kupewa zawadi “ni jambo la faraja pale mtu
anapostaafu wenzio wakakuaga na kukuandalia tafrija fupi inapendeza na
kujisikia kama wenzangu wananijali wananipenda na wananiombea mazuri” .
Naibu Seif
amesema mafunzo kwa wastaafu yanasaidia kujiimarisha mapema ili kuondokana na
khofu iliyojengeka kwa baadhi yao pamoja na kujiwekeya mazingira mazuri ya
kujiendeleza watakapokuwa nje ya Ofisi mara baada ya kustaafu
Mkurugenzi wa
uendeshaji na utumishi ndugu Bakari Khamis
Muhidin amesema ofisi ina kila sababu za
kuwatunukia vyeti na zawadi za ukumbusho kutokana na utendaji wao mzuri katika
kuitumikia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Kwa niaba ya
wastaafu ndugu Ali Shaaban amesema suala la mafunzo ya kujitayarisha kustaafu
ni muhimu hivyo ni vyema jambo hilo kutiliwa mkazo na kuendelezwa kwani kwa upande wake ameiona faida ya kupata
mafunzo hayo.
Nao wafanyakazi
wa Ofisi hio katika risala ya kuwaaga wafanyakazi hao wamewapongeza kwa kufikia hatuwa ya kustaafu
wakiwa wamemaliza muda wao wa utumishi wakiwa na afya njema yenye furaha ingawa
ni masikitiko kwa kutokuwa nao kwani tayari walikuwa ni familia moja hivyo wamewaomba
wastaafu hao kutokana na uzowefu wao wa kazi
kutowaacha mkono bali wawe tayari kutumia busara zao hekima na ujuzi
pale watakapohitajika .
Aidha wameahidi
kwa Mhe Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohamed
Shein ambae ndio Kiongozi mkuu wa Ofisi
ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuendelea kufanya kazi
kwa taratibu zote na sio kwa mazowea kwani wanaongozwa na Mkataba wa Utoaji
Huduma kwa Umma
Wafanyakazi hao
waliostaafu wamefanya kazi katika kada tofauti na taasisi mbalimbali na hatimae kumalizia Ofisi ya Rais Katiba
Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora jumla yao ni saba ambapo wametunukiwa
vyeti, fedha taslim na zawadi nao ni Bw
Omar Khamis Shaaban, Bi Asha Ali Omar, Bw Silima Khamis Daima, Bw Ali Shaaban
Masoud Bw Joseph Antony Mussa, Bw Rashid Amour Alley na Bw Mohamed Khamis.
No comments:
Post a Comment