Habari za Punde

Kikao cha Kawaida Cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Kifenyanyika Leo Jijini Dar es Salaam Chini ya Mwenyekiti Wake Mhe. Dkt. John Magufuli ykIKAO . na Kuwarejeshea Uwanachama Wao Wanachama Wanne wa CCM.

Wanachama hao waliosamehewa wakiwa wamesimama mbele ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu Mwenyekiti wake Ndg. Philip Mangula na Katibu Mkuu Dkt. Bashiru Ally na mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC) wakati wa  Kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa leo tarehe Desemba 18, 2018 Jijini Dar es Salaam 

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ofisi Ndogo ya Makao Makuu Lumumba.
18 Desemba, 2018

Kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kimefanyika leo tarehe 18 Desemba, 2018 Jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Ndg. John Pombe Joseph Magufuli, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kikao hicho kimepokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kutoka kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na taarifa ya chama juu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa CCM ya mwaka 2015.

Pia, kikao hicho kimepokea taarifa kuhusu masuala ya maadili, kimepokea na kuridhia marekebisho ya kanuni mpya za fedha na mali za chama na jumuiya zake na kimepokea na kuridhia uteuzi wa wajumbe wa Baraza la Wadhamini wa CCM.

Kwa kauli moja Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imepokea maombi na kukubali kusamehewa adhabu ya kufukuzwa uanachama kutoka kwa waliokuwa wana CCM wanne ambao walitenda makosa hayo wakiwa Wenyeviti wa CCM ngazi ya Mikoa na Wilaya.

Waliosamehewa na kurejeshewa uanachama ni;

1.    Ndg. Ramadhani Rashid Madabida (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam).
2.    Ndg. Erasto Izengo Kwirasa (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga).
3.    Ndg. Christopher Mwita Sanya (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara).
4.    Ndg. Salum Kondo Madenge (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni).

Aidha, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kauli moja imeamua kumuweka katika uangalizi Ndg. Jesca Msambatavangu ambaye ameomba kurejeshewa uanachama wa CCM baada ya kufukuzwa kwa makosa ya kimaadili.

Halikadhalika, Halmashauri Kuu ya CCM imepitisha majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama katika ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa zilizoachwa wazi baada ya waliokuwa katika nafasi hizo kupangiwa majukumu mengine ya Kiserikali au  kufariki dunia pamoja na mgombea wa CCM wa kiti cha Ubunge katika Jimbo la Temeke Jijini Dar es Salaam.

Waliopitishwa kugombea nafasi hizo ni kama ifuatavyo.

1.    Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
                     i.        Dkt. Damas Mukasa Kashegu
                    ii.        Asha Juma Feruzi
                   iii.        Galila Ramadhani Wabanhu
                  iv.        Makene Pamella Boniphas

2.    Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa
                     i.        Dkt. Abel Mwendawile
                    ii.        Aman Said Mwamwindi
                   iii.        Sabas Vitus Mushi

3.    Katibu wa Itikadi na Uenezi Mkoa wa Simiyu
                     i.        Mashaka Abeid Makongoro
                    ii.        Mayunga Genga Ngokolo
                   iii.        Heri Mchunga Zebedayo

4.    Mwenyekiti wa Wazazi Mkoa wa Mwanza
                     i.        Bahebe Emmanuel Ezekiel
                    ii.        Nyiriza Makongoro Nyiriza
                   iii.        Masso Gerald Jane
                  iv.        Misogalya Isaac Kilangi Kassile

5.    Mwenyekiti wa Wazazi Mkoa wa Mwanza
                     i.        Salum Mohamed Chima
                    ii.        Yusuph Mwandami Gwayaka
                   iii.        Bertha Peter Nakomolwa
                  iv.        Philemon Josephat Kiemi

6.    Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kibaha Mjini
                     i.        Amina Ally Kobo
                    ii.        Lemmy Joel Ludovick
                   iii.        Hamidi Rajabu Shebuge
Halmashauri Kuu ya CCM imemteua Ndg. Abdallah Ally Mtolea kuwa Mgombea wa kiti cha ubunge kwa tiketi ya CCM katika Jimbo la Temeke, Jijini Dar es Salaam.

Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imeiagiza Jumuiya ya Umoja wa Vijana (UVCCM) kurudia mchakato wa kupendekeza majina ya mgombea wa nafasi ya Mjumbe wa NEC.

Wakati huo huo, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kauli moja imetupilia mbali pingamizi zilizowekwa dhidi ya viongozi wa CCM katika ngazi mbalimbali na kuagiza viongozi hao waendelee na nyadhifa zao.

Pingamizi hizo ziliwekwa dhidi ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndg. Anthony Mwandu Diallo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Mkoa wa Lindi Ndg. Aisha Ally, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Ndg. Salim Mohamed na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ngara Ndg. George Jackson Rubagora.

Pamoja na kutupilia mbali pingamizi hizo, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imewaagiza walezi wa mikoa yote ambayo viongozi wake waliwekewa pingamizi wakutane na wanachama na kukiunganisha chama.

Halmashauri Kuu ya CCM imemuagiza Ndg. Zubeir Majaliwa (aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Uvinza) ambaye Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Uvinza ilimsimamisha uanachama kuwasilisha rufaa yake kuanzia ngazi husika wakati adhabu yake ikiendelea.

Aidha, Halmashauri Kuu ya CCM imetoa adhabu ya KALIPIO kwa mwanachama wa CCM Ndg. Hasnain Murji kutokana kukabiliwa na makosa ya kimaadili.



Ndg. Bashiru Ally Kakurwa
Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.