Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye (kushoto)
akimvua cheo cha zamani na kumvisha cheo kipya cha Kamishna wa Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji (CF) Mbaraka Semwanza katika ukumbi wa mikutano Ofisi za
Makao Makuu ya Jeshi Dar es salaam mapema leo asubuhi tarehe 11/12/2018
Kamishna
(CF) Mbaraka Semwanza akiapa baada ya kuvishwa cheo kipya cha Kamishna wa
Utawala na Fedha wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika ukumbi wa mikutano
Makao Makuu ya Jeshi hilo mapema leo asubuhi
Kamishna
wa Utawala na Fedha (CF) Mbaraka Semwanza (kushoto) akipokea nyaraka mbalimbali
za ofisi ya Utawala na Fedha kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto
na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye (kulia), baada ya kuapishwa katika ukumbi
wa mikutano Makao Makuu ya Jeshi hilo mapema leo asubuhi
Makamishna,
Wakuu wa Vitengo, Maafisa na Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
wakishuhudia kuapishwa kwa Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi hilo, katika
ukumbi wa mikutano Makao Makuu ya Jeshi hilo mapema leo asubuhi
NA
KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA - JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MAKAO MAKUU
No comments:
Post a Comment