Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu akihutubia wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Sheria Zanzibar, zilizofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete Kisiwani Pemba.
Na.Abdi Shamna -Pemba.
JAJI mkuu wa
Zanzibar. Omar Othman Makungu amesema taasisi za umma zinathamni mchango mkubwa
wa serikali katika kufanikisha mageuzi ya kutendaji, ili kufanikisha dhana ya utoaji
bora wa haki katika jamii.
Amesema
taasisi hizo, ikiwemo mahakama, Ofisi ya Mwendesha mashtaka, pamoja na Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu zinaridhishwa na juhudi zinazochukuliwa na serikali katika
kuimarisha miundombinu, upatikanaji wa vifaa pamoja na mafunzo kwa watendaji.
Jaji mkuu
amesema hayo leo katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, wakati akitoa nasaha
zake katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Sheria Zanzibar.
Maadhimisho
ya Siku ya Sheria Zanzibar yanaakisi kuanza kwa mwaka mpya wa sheria hapa
Zanzibar.
Alisema
kutokana na mchango huo shughuli za Mahakama zimeimarika, hususan baada ya Serikali
kuteuwa Majaji, mahakimu na makadhi wapya katika ngazi zote za mahakama Unguja
na Pemba.
Alisema kwa
nyakati tofauti watendaji wa taasisi hizo wamepata mafunzo ya ndani na nje ya
nchi, hivyo kujenga uwezo katika kufanikisha dhana ya serikali ya upatikanaji
wa haki bora kwa jamii.
Aidha,
aliipongeza Serikali kwa kuimarisha mhimili huo wa Dola (mahakama) kimuundo na
kibajeti , sambamba na hatu ya kuanzisha mfuko wa mahakama, ambao utaiwezesha
taasisi hiyo kufanyakazi zake kwa ufanisi zaidi.
Jaji Othman
aliipongeza serikali kwa kuanzisha mradi wa usalama na kufunga kamera za CCTV,
hatua itakayosaidia sana kuimarisha usalama wa mji pamoja na kubaini makosa mbalimbali,
yakiwemo ya usalama barabarani, hivyo kuipunguzia kazi mahakama.
Jaji
Othaman, alipongeza azma ya serikali ya kuanzisha ujenzi wa jengo jipya la
mahakama kuu katika eneo la Tunguu, litakaloambatana na skuli ya mafunzo ya
sheria ‘Law school’.
Aidha,
Waziri wa Wizara ya Nchi (OR) katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Haroun Ali Suleiman aliwapongeza viongozi wa Serikali wa Mikoa na Wilaya
kisiwani Pemba kwa mashirikiano makubwa yaliofanikisha vyema sherehe hizo.
Nae,
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Said Hassan Said alisema uimarishaji wa taasisi za
umma utarahisisha upatikanaji wa haki katika suala zima la Utawala Bora.
Alisema
changamoto iliopo kwa baadhi ya watendaji wa taasisi za umma, inatokana na
ukosefu wa utaalamu, weledi na ukiukwaji wa maadili .
Alisema kuna
umuhimu wa kuimarisha mfumo ili kuwajengea zaidi uwezo watendaji wa taasisi
hizo ili hatimae waweze kufanyakazi zao kwa ufanisi.
Alisema
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu itashirikiana na taasisi zote za umma pamoja na wadau
wa sheria kufanikisha malengo ya kuwepo kwake.
Alisema ni
mpango wa Ofisiya Mwanasheria mkuu kufungua
Ofisi kisiwani Pemba katika mwaka huu wa fedha 2019/2020, sambamba na kuendesha
program ya ‘outreach’ ili wananchi waweze wafaidika na huduma za kisheria.
Mapema,
Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP), Ibrahim Mzee alisema utatuzi wa
migogogro kupitia mifumo isiyo rasmi, hususan ule wa kujichukulia sheria
mikononi ina madhara makubwa kwa jamii.
Alisema
suala la upatikanaji wa haki ni kiashiria muhimu katika maendeleo ya watu
kiuchumi na kijamii.
Alisema
Ofisi ya DPP itaendelea kushirikiana na tasisi nyengine za umma, ili
kufanikisha dhana ya upatikanaji wa haki, ili jamii iweze kupata haki kwa
usawa.
Aidha,
Mwakilishi wa Chama cha Wanasheria Zanzibar Omar Said Shaaban, alisema mjumuiko
huo unatowa fursa kwa wadau wa sheria kukumbusha changamoto zinaoikabili sekta
hiyo na jamii kwa jumla ili kuzipatia ufumbuzi.
Alisema ipo
haja ya kuziimarisha taasisi zote, ikiwemo za binafsi ili kuondokana na
changamoto mbali mbali katika suala zima la upatikanaji wa haki.
Aidha alisema
wakati umefika kwa Zanzibar kuwa na chama chake ‘ Zanzibar Law Society’ kwa mujibu wa sheria zitakazopitishwa na
Baraza la Wawakilishi, ili kuweza kutekeleza wajibu wake kisheria.
Maadhimisho
hayo yalioambatana na kauli mbiu “uimarishaji wa Taasisi za Umma ni Ustawi bora
wa Upatikanaji wa Haki kwa jamii”, yalihuduriwa na Majaji, Mahakimu, Makadhi,
Masheha, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama pamoja na
wadau wengine wa sheria kutoika mikoa ya Unguja na Pemba.
No comments:
Post a Comment