Naibu
Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza akijibu
swali la Mbunge wa Konde Mhe.Khatib Haji (CUF) kuhusu mgao wa fedha za FIFA
zinazopelekwa TFF na utaratibu unaotumiwa na TFF kuwapatia fedha hizo Chama cha
Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) leo Bungeni jijini Dodoma.
Na Anitha Jonas - WHUSM. -Dodoma.
Serikali kwa
kushirikiana na taasisi zote muhimu imejiandaa kupokea wageni wote watakao
shiriki mashindano ya AFCON yanayotarajia kufanyika nchini hivi karibuni .
Kauli hiyo imetolewa
leo bungeni jijini Dodoma na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipokuwa
akijibu swali la Mbunge wa Kilolo Venance Mwamoto (CCM) wakati wa maswali ya papo
kwa papo ya wabunge.
"Serikali
inatambua maandalizi yanayofanyika na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na
Michezo kwa kushirikiana na Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) pamoja na wadau mbalimbali na tunatambua kuwa tutapokea wageni wengi
akiwemo Rais wa Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA)",alisema Mhe.Waziri
Mkuu Majaliwa.
Aidha,Mheshimiwa
Waziri Mkuu aliendelea kusema kuwa kupitia mashindano hayo serikali
imehamasisha Mikoa ya jirani kujipanga kunufaika na mashindano hayo na jumla ya
viwanja vitatu vitatumika na nijukumu la watanzania wote kushirikiana ili kuhakikisha
tunanufaika kwa ujio huu mkubwa.
Pamoja na hayo Mheshimiwa
Majaliwa aliendelea kuwasisitiza TFF kuimarisha maandalizi ya timu hiyo itayoshiriki
ili taifa liweze kuibuka kidedea,vilevile aliwasihi watanzania wote kuonyesha
uzalendo kwa timu yao ili kuweza kuwatia moyo kwa kuwa na imani kuwa timu hiyo itaweza kushinda.
Nae Naibu Waziri Wizara
ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza ametoa majibu ya swali
la Mbunge wa Konde Mhe.Khatibu Haji (CUF) lilihoji kuhusu mgao wa fedha zinazotolewa
na FIFA kwa TFF kuwa ni kiasi gani zimekwisha pelekwa kwa Chama cha Mpira wa Miguu
Zanzibar (ZFA) kwa kusema kuwa kuwa kufuatia changamoto TFF kutokukidhi vigezo
vya utawala bora na uwazi katika matumizi ya fedha kwa zaidi ya miaka mitatu
wamekuwa hawapati mgao na FIFA ila kwa kuanzia mapema mwaka huu wanatarajia
kuanza kupata mgao huo baada ya kutatua changamoto hizo.
Halikadhalika katika swali
la nyongeza Mhe.Naibu Waziri Shonza alijibu kuwa si kweli kuwa ZFA haijawahi
kupatiwa msaada wa TFF kwani wameshawahi kupatiwa msaada wa miradi moja wapo ni
ujenzi wa ukarabati wa uwanja wa Gombani Pemba na kufafanua kuwa ZFA ni sehemu
ya TFF hivyo fedha zinazoletwa na FIFA kwa TFF hugawiwa kwa mashirikisho yote na ZFA hawaletewi fungu
lao peke yao kwani ZFA siyo mwanachama FIFA wala CAF.
No comments:
Post a Comment