Habari za Punde

Timu ya Villa Uniteds Inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Kanda ya Unguja Yajitoa.

Rais wa Timu ya Villa Uniteds Abdulrabi Mahfoudh (Manji)akizungumza na waandishi wa habari za Michezo kuhusiana na kujitowa kwa  Timu yake katika Michuano ya Ligi Daraja  la Kwanza Unguja,akizungumza katika ukumbi waKlabu yao Mwanakwerekwe Unguja leo.

Na. Hawa Ally, Zanzibar.
UONGOZI wa timu ya Villa Uniteds “Mpira Pesa “umeamua kuivunja na kuifuta timu hiyo iliyokuwa ikishiriki ligi daraja la kwanza Kanda ya Unguja kwa kuwatuhumu baadhi ya waamuzi na viongozi wa ZFF kuifanyia hujuma timu hiyo.
Akizungunmza na Waandishi wa habari Rais wa timu hiyo Abdurabi Dau “Manji” alisema baadhi ya waamuzi wanashindwa kuzitumia sheria 17 za mpira kama zilivyo badala yake wamekuwa wakifanya upendeleo kwa baadhi yatimu.
Alisema baadhi ya waamuzi wamekuwa wakifungisha magoli ambayo unaona kabisa sio magoli halali  nah ii  inatokana na mambo mawili aidha vitendo vya rushwa pamoja na kufanya upendeleo kwa timu hususani zile za vikosi.
Aidha alisema walishapeleka malalamiko yao katika chama cha soka Zanzibar ambacho sasa ni shirikisho lakini hakuna jitihada ambazo zilizowezwa kuchukuliwa badala yake timu hiyo inaendelea kuhujumiwa jambo ambalo wachezaji na hata viongozi hawaliridhiki nalo.
Alisema  maaamuzi ya kuivunja  timu hiyo hayakuwa ya viongozi tu bali hata wachezaji waliokuwa wakiitumikia timu hiyo walichoshwa na vitendo hivyo ambavyo vinasababisha hata kurejesha nyuma jitihada zao za kuona kama soka ni ajira kama  zilivyo ajira nyingine.
“Mpira unauma husususani pale unaoona umeonewa hasa , maana tunatumia pesa nyingi kwa kuhidumia tumu, kusajili wachezaji alafu ukija kukuta mambo hayayunayofanyiwa ya kufungishwa kwa makusudi kwakweli jambo hili tumechoka kulivumilia.”Alisema.
Aidha alisema wachezaji wawili  waliwasajili kutokea Tanzania bara  ambao ni Shabani Abdalla na Mohmed Abdul wanafanya utaratibu wa kuwarejesha kwao ili wakajiendeleze zaidi na soka kwani viwango vyao ni vyakuridhisha.
Rais huyo wa Vila United  alisema kuwa  anatarajia kuwasilisha barua kwa shirikisho la soka ZFF na kwa mrajisi juu ya kuifuta na kuivunja timu hiyo na haitakuwepo tena.
Timu hiyo ya Villa United hadi inavunjwa ilikuwa imebakisha mchezo mmoja wa kumaliza msimu  na ilikuwa katika nafasi ya 3 na alama 57 katika msimamo wa ligi daraja la Kwanza Kanda ya Unguja.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.