Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa akiwa na mtoto mwenye Ulemavu Happy Shabani Salumu mara baada ya kukabidi msaada wa baiskeli kwa mtoto huyo
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa akimkabidhi baiskeli mtoto Happy Shabani Salumu, ambaye ni mlemavu wa viungo itakayo msaidia kwenda shuleni na kumwezesha kufanya shughuli nyingine kwa urahisi. Kulia ni Mzazi wa mtoto huyo Bi. Magreth Leo.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Watu wenye Ulemavu Bi. Josephine Lyengi akizungumza na mzazi wa Mtoto huyo Bi. Magreth Leo.
Baadhi ya Maafisa wa Kitengo cha Huduma kwa Watu wenye Ulemavu wakifuatilia maelezo ya Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa (hayupo pichani) alipokuwa akitoa msaada wa baiskeli kwa mtoto Happy Shabani Salumu. Kushoto ni Afisa Ustawi wa Jamii Bi. Joy Maongezi na Bi. Oliver Njogopa (katikati).
Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana Ajira na Wenye Ulemavu)
No comments:
Post a Comment