Mwenyekiti wa mashindano ya Ritta Kabati challenge cup 2019 Gerald Malekela akizungumza na waandishi wa habari wa mkoani Iringa juu zoezi la uchukuaji wa fomu za mashindano hayo.
Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo msimu wa pili wa mwaka 2018 /2019 (Picha kutoka maktaba)
Kamati anzilishi ya mashindano ya Ritta Kabati Challenge Cup toka msimu wa kwanza mwaka 2017 (picha kutoka maktaba)
NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
Kamati ya ya mshindano ya Ritta Kabati challenge cup 2019 imezindua rasmi kwa kuanza kuzialika timu kwa ajiri ya kuchukua fomu kushiriki na wameweka bayana jinsi mfumo wa mashindano utakavyokuwa pamoja na zawadi kwa washindi wote.
Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa mashindano hayo Gerald Malekela alisema msimu wa tatu wa mashindano Makubwa kwa ukanda
huu wa nyanda za juu kusini ya Iringa Challege Cup ambayo yanadhaminiwa na Mbunge
viti maalum Mkowa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Ritta Kabati
unazinduliwa rasmi kwa kwa timu kuanza kuchukua fomu za usajili kwa kulipa ada
ya shilingi 50,000 na fomu zinapatikana katika
kituo cha radio cha Nuru Fm.
Malekela alisema kuwa zoezi la uchukuaji fomu na
kurudisha limenza rasmi tarehe 14 mwezi huu na litafikia kikomo tarehe 25 mwezi
huu wa tano na baada ya hapo mchakato wa kupitia usajili na upangaji wa ratiba ya
mechi itafanyika na baada ya hapo tunatarajia kuzindua rasmi tarehe 1 au 2 ya
mwezi wa sita yaani mwezi ujao
“Fomu zinapatika kwa
kamati wanaweza wakawasiliana na katibu kwa namba 0742483733 Au mwenyekiti Mimi
hapa 0715779233 au wafike Nuru fm watapata na wale waliombali bado unaweza
ukatumia fomu baada ya kutuma ada 50,000 tunakutumia mnajaza mnarejesha” alisema
Malekela
Aidha Malekela alisema kuwa matarajio ya kamati msimu
huu ni kuwa na timu chache ili kufanya vizuri katika mashindano hayo na
makadilio kupata timu 40 kwa Mkoa mzima. Msimu wa mwaka jana tulikuwa na timu
zipatazo 67 na kamati ilipambana na mashindano yakaisha bila kuwepo tatizo
lolote licha ya kasolo ndogondogo ambazo ni udhaifu wa kibinadamu.
Malekela
alisema kuwa lengo la mashindano ni kuibua vipaji vya vijana mkoani
Iringa,Kuonesha uwezo wa
vijana na kutengeneza ajira kwao,Kujenga kizazi chenye afya bora na kuwa na utamaduni wa kufanya mazoezi,Kutoa burudani kwa wakazi wa iringa kwa mchezo
wa mpira wa miguu,Kuwakutanisha vijana pamoja ili kuzungumza lugha moja ya kimichezo na maendeleo,Kuwaepusha vijana na makundi au vijiwe visivyo faa na
Kuhamasisha michezo katika mkoa wa Iringa,kutimiza
agizo la makamu wa raisi juu ya kufanya
mazoezi
“Sasa hapo
utagundua kuwa jinsi gani mashindano hayo yalivyo yanaumuhimu katika kukuza vipaji hapa mkoani kwa ustawi wa soka letu la nchi hiii” alisema Malekela
Lakini Malekela alizitaja
zawadi pamoja ambazo zitatolewa kwa timu shiriki
No.
|
Muhusika
|
Zawadi
ya kwanza
|
Zawadi
ya pili
|
1.
|
Mshindi wa kwanza
|
Kombe
|
2,000,000.00
|
2.
|
Mshindi wa pili
|
1,000,000.00
|
|
3.
|
Mshindi wa tatu
|
500,000.00
|
|
4.
|
Mchezaji bora
|
100,000.00
|
|
5.
|
Mfungaji bora
|
100,000.00
|
|
6.
|
Golikipa bora
|
100,000.00
|
|
7.
|
Waamuzi bora
|
100,000.00
|
|
8.
|
Ushangiliaji bora
|
200,000.00
|
|
9.
|
Timu yenye nidhamu
|
100,000.00
|
|
Jumla
|
4,200,000
|
Ligi yetu itakuwa kama msimu uliopita tutakuwa na hatua ya mtoano kulingana na timu zitakazo jitokeza kuchukua fomu za kushiriki mashindano haya na hatimaye kupata timu kumi ambazo zitacheza hatua ya makundi mawili na kupata timu nne ambazo zitacheza nusu fainali na hatimaye fainal
Kama kamati tunamshuru sana Mh.Mbunge Ritta Kabati kwa kukubali kudhamini mashindano haya na kuwathamini
vijana wa mkoa wa Iringa fedha hii
ambayo anaitoa kwaajili ya kufanya yote haya angeitumia kwa kazi zake nyingine kwa maendeleo ya familia yake lakini kwa kutambua nafasi aliyonayo na kuwathamini vijana ndio maana anafanya haya yote hivyo sisi kamati tunamshukuru na kumpongeza aendelee kuwa na moyo huu.
No comments:
Post a Comment