RAIS wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewatumia salamu za
pongezi Rais wa Rwanda Paul Kagame na Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kwa
kutimiza miaka 57 ya Uhuru wa Mataifa hayo.
Katika salamu ambazo Rais Dk. Shein amemtumia Rais
wa Rwanda Paul Kagame zilieleza kuwa kwa niaba ya wananchi wa Zanzibar wanaungana
pamoja na ndugu zao wa Rawanda katika kusherehekea siku hii muhimu katika
historia ya Taifa hilo.
Salamu hizo zilipompongeza Rais Kagame kwa
jitihada kubwa alizozichukua katika kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi hiyo
sambamba na kuimarika kwa mshikamano wa wananchi wa Taifa hilo.
Aidha, salamu hizo, zilieleza kuwa tukio hilo
kubwa, linatoa nafasi ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano mkubwa kati ya pande
mbili hizo pamoja na wananchi wake hatua ambayo itaimarisha zaidi uhusiano
katika nyanja za Kitaifa na Kimataifa yakiwemo mashirikiano katika Jumuiya yao
ya nchi za Afrika Mashariki (EAC).
Sambamba na hayo, Dk. Shein alimtakia kiongozi
huyo pamoja na familia yake na wananchi wote wa Rwanda, afya njema na kuwatakia
sherehe njema zenye amani na utulivu wananchi wa nchi hiyo.
Wakati huo
huo, Rais
Dk. Shein pia, alitumia salamu hizo za pongezi Rais wa Burundi Pierre
Nkurunziza kwa kutimiza miaka 57 ya Uhuru wa Taifa hilo na kueleza kuwa
wananchi wa Zanzibar kwa niaba yake wanaungana na ndugu zao wa Burundi katika
kusherehekea uhuru wa Taifa hilo.
Salamu hizo zilieleza historia na uhusiano
sambamba na mashirikiano yaliopo kati ya Zanzibar, Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Burundi na kueleza jinsi inavyojivunia mafanikio yaliopatikana
nchini Burundi tokea kupatikana kwa uhuru wake.
Aidha, salamu hizo zilieleza kuwa hatua hiyo ni
bahati kubwa inayoashiria mashirikiano na mahusiano mema ya kidugu kwa nchi wanachama
wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC).
Katika salamu hizo, Rais Dk. Shein pia, alimtakia
kiongozi huyo pamoja na familia yake na wananchi wote wa Burundi, afya njema na
kuwatakia wananchi wa hiyo kusherehekea kwa
amani na utulivu siku hii adhimu na ya kihistoria ya nchi hiyo.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment